LIVE STREAM ADS

Header Ads

WANAHABARI NCHINI WATAKIWA KUONDOA IMANI POTOFU KUHUSU RUZUKU ZA TMF.




Na BMG
Wakfu wa Tasnia ya Vyombo vya Habari nchini (TMF), umekutana na Waandishi wa Habari mkoani Mwanza kuwapa ufafanuzi kuhusu ruzuku zake.


TMF inatoa ufafanuzi kwa wanahabari hao kuhusu namna ya kuomba ruzuku kwa ajili ya kuwezesha kutimiza majukumu yao ya kuandika habari na makala mbalimbali zenye tija kwa jamii.

Dastan Rafael kutoka TMF amewahimiza Wanahabari kutumia fursa hiyo ili kuomba ruzuku na kuondokana na mawazo hasi kwamba ruzuku hizo hutolewa kwa upendeleo ambapo kuanzia mwakani TMF itaanza kupokea maombi ya ruzuku kutoka kwa wanahabari na taasisi za vyombo vya habari.

Hata hivyo baadhi ya Wanahabari wameiomba TMF kupunguza mchakato mrefu wa mfumo wa mtandaoni wa kujaz fomu za uombaji wa ruzuku zake kwani hatua zake zimekuwa zikisababisha asilimia kubwa ya wanahabari kutoomba ruzuku hizo. 

No comments:

Powered by Blogger.