LIVE STREAM ADS

Header Ads

BODI YA FILAMU NCHINI YAENDELEA KUWANOA WANATASNIA WA FILAMU MKOANI MARA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba, akiongozana na Naibu Katibu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Milla pamoja na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fisso, kwenye ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu kwa Wanatasnia wa Filamu na michezo ya kuigiza mkoani Mara, yaliyoanza jana kwenye ukumbi wa shule ya Sekondari Mara Mjini Musoma.

Mafunzo hayo yamelenga kukuza weledi kwa wazalishaji wa filamu na maigizo ikiwemo kuzingatia uandishi bora wa miswada ili kuendana na ushindani wa soko la ndani na nje ya nchi.
#BMGHabari
Naibu Katibu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Milla (kulia) akiteta jambo na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fisso, kwenye ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu kwa Wanatasnia wa Filamu na michezo ya kuigiza mkoani Mara.
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fisso (kushoto), pamoja na Kaimu Afisa Utamaduni mkoani Mara, Shekudadi Said (kulia), wakiwa kwenye ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu kwa Wanatasnia wa Filamu na michezo ya kuigiza mkoani Mara.
Naibu Katibu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Milla (kulia), Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fisso (kushoto) pamoja na wanatasnia wa filamu na maigizo mkoan Mara wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo.
Mmoja wa Wakufunzi wa mafunzo hayo, Richard Ndunguru kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam idara ya Sanaa, akitoa mafunzo kwa wanatasnia wa filamu na maigizo mkoani Mara. Amewapa miongozo bora kuhusiana na uandishi wa miswada ya filamu, upigaji wa picha mnato pamoja na nyongevu kwa ubora zaidi ili kuongeza mvuto wa kazi zao.
Wanatasnia wa filamu na maigiozo mkoani Mara, wakifuatilia kwa umakini mafunzo kutoka kwa Richard Ndunguru ambaye ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam idara ya Sanaa.
Wanatasnia wa filamu na maigiozo mkoani Mara, wakifuatilia kwa umakini mafunzo hayo.
Wanatasnia wa filamu na maigiozo mkoani Mara.
Wanatasnia wa filamu na maigiozo mkoani Mara wakiwa kwenye mafunzo ya filamu na maigizo mkoani humo, yanayotolewa na Bodi ya Filamu nchini.
Taswira ndani ya ukumbi wa mafunzo hayo.
Soma Zaidi HAPA

No comments:

Powered by Blogger.