MCHUNGAJI SALAGE WA PENTEKOSTE KAWEKAMO JIJINI MWANZA ALIA NA SUALA LA AMANI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand, Mwanza
Waamini wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini wameombwa kutunza amani iliyopo ili kuweza kufanya mambo kwa utulivu, hivyo kutasaidia kuleta maendeleo na kukuza uchumi.
Ushauri huo ulitolewa jana na Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste lililopo Kawekamo B wilayani Ilemela mkoani Mwanza, Emmanuela Salage.
Alisema, kwa kudumisha amani na upendo ni vema waumini wakamtanguliza Mungu katika kazi zao ili kuweza kuepuka kufanya vitendo viovu.
Pia alisema, ni vema wananchi wakawa na utaratibu wa kufichua watu ambao wanafanya vitendo vya uhalifu katika maeneo yao, ili waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria kwani kuvunja amani siyo jambo jema, kunasababisha jamii kushindwa kufanya shughuli za kuwapatia kipato.
“Tunatakiwa kujiandaa wakati wote kwa kufanya mambo mema ambayo yanayompendeza muumba wetukwani hakuna ajuaye siku ya kifo sambamba na kutunza amani ya nchi hii iliyotafutwa kwa kipindi kirefu,”alisema Salage.
Judith Ferdinand, Mwanza
Waamini wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini wameombwa kutunza amani iliyopo ili kuweza kufanya mambo kwa utulivu, hivyo kutasaidia kuleta maendeleo na kukuza uchumi.
Ushauri huo ulitolewa jana na Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste lililopo Kawekamo B wilayani Ilemela mkoani Mwanza, Emmanuela Salage.
Alisema, kwa kudumisha amani na upendo ni vema waumini wakamtanguliza Mungu katika kazi zao ili kuweza kuepuka kufanya vitendo viovu.
Pia alisema, ni vema wananchi wakawa na utaratibu wa kufichua watu ambao wanafanya vitendo vya uhalifu katika maeneo yao, ili waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria kwani kuvunja amani siyo jambo jema, kunasababisha jamii kushindwa kufanya shughuli za kuwapatia kipato.
“Tunatakiwa kujiandaa wakati wote kwa kufanya mambo mema ambayo yanayompendeza muumba wetukwani hakuna ajuaye siku ya kifo sambamba na kutunza amani ya nchi hii iliyotafutwa kwa kipindi kirefu,”alisema Salage.
No comments: