LIVE STREAM ADS

Header Ads

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AKAGUA UJENZI WA HOSPITALI YA MAMA NA MTOTO CHANIKA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Displaying RC-MAKONDA-CHANIKA-6.jpgJames Salvatory, BMG Dar
Mkuu mkoa wa Dar es salaam, Paulo Makonda, jana amefanya ziara kukagua ujenzi unaoendelea  katika hospital ya mama na mtoto iliyopo eneo la Chanika na ambayo itawahudumia wakazi wa eneo hilo na maeneo jirani waliokuwa  wakilazimaka kutembea umbali mrefu  kufuata huduma za afya katika hospitali ya Amana na Muhimbili.

Akizungumza mara baada ya kukagua hospitali hiyo Makonda  alisema kuwa hospitali hiyo itakuwa na vitanda 160 na itakuwa inahudumia wagojwa 1000 kwa siku, na vikiwa na vyumba viwili  vya upasuaji vyenye uwezo wa  kuhudumia wagonjwa wagonjwa wanne  kwa kila chumba   huku kukiwa na Watumishi zaidi ya 150 ambao watakuwa wakiishi hapo hapo karibu na hospitali hiyo kwani ujenzi wa hospitali hiyo unaendana  na makazi wa wafanyakazi.

"Nimeshangaa na kufurahi Mara baada ya kukuta ujenzi ukiwa umefikia sehemu nzuri maana nilikuja kuweka jiwe la msingi mwezi wa tatu mwaka huu  na kwa muda uliopita ni wazi kabisa kazi inafanyika kwa ufasaha mkubwa," alisema Makonda.

Mradi huo ambao umefadhiriwa na shirika la maendeleo   ya Korea ya kusia (KOICA), ukiwa umegharimu billion nane na million mia nane mpka kukamilika kwake na unategemewa kukamilika mwezi februari mwakani.

No comments:

Powered by Blogger.