LIVE STREAM ADS

Header Ads

PSPF WAKABIDHI VITAMBULISHO KWA WANACHAMA WAPYA WALIO JIUNGA KUPITIA MAONYESHO YA VIWANDA JIJINI DAR.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Uwekezaji  Dkt. Adelhelm Meru(kushoto) akiwa katika Banda la Mfuko wa Pensheni wa PSPF wakati wa kufunga Maonesho ya viwanda viwanja vya sabasaba.
Blog za Mikoa
 Meneja wa Mpango wa Uchangiaji wa Hiari wa  mfuko wa PSPF Bi. Mwanjaa Sembe akitoa maelezo mbalimbali juu ya Mfuko huo.
Kulia Afisa Mwendeshaji Mfuko wa Pensheni wa PSPF Hadji Jamadary akitoa elimu kwa Mwananchi kuhusiana na uchangiaji wa hiari huku akimwonyesha bango lililo orodhesha mafao yanayo tolewa na PSPF kupitia PSS.

 Wananchi mbalimbali wakiwa wametembelea banda la mfuko wa pensheni wa PSPF kwaajiri ya kujifunza shughuli zinazofanywa na mfuko huo.
 Mmoja wa wananchi walio fika na kujisajiri na mfuko wa PSPF akijaza fomu ya kujiunga na mpango wa uachangiaji wa hiari (PSS).
 Afisa Mwendeshaji Mfuko wa Pensheni wa PSPF Hadji Jamadary akikabidhi vitambulisho kwa badhi ya wanachama walio jiunga na mpango wa uchangiaji kwa hiari katika maadhimisho ya maonyesho ya viwanada jijini dar
 Afisa Mwendeshaji Mfuko wa Pensheni wa PSPF Asmahan haji akiendelea kufanya shughuli za kiofisi katika banda la PSPF ndani ya maonyesho ya viwanda (saba saba) jijini Dar es salaam.
Meneja wa Mpango wa Uchangiaji wa Hiari wa  mfuko wa PSPF Bi. Mwanjaa Sembe (Kushoto), akiwapa vitambulisho wanachama waliojiunga na mfuko huo kupitia uchangiaji wa hiali (PSS)

Mfuko wa Pensheni wa PSPF wahitimisha maonyesho ya viwanda vidogovidogo na  wajasiliamali  kwa kugawa vitambulisho kwa watu walio jiunga na mfuko huo katika uwanja wa maonyesho ya biashara waMwl.J.K Nyerere (saba saba) jijini Dar es salaam.

Maonyesho hayo yaliyodumu kwa takribani siku tano ambapo yalianza Tareh 5.12.2016 na kuhitimishwa  Tarehe 11 /12/2016 yakiwa na kauli mbiu isemayo ‘TANZANIA SASA TUNAJENGA VIWANDA’ PSPF walikuwa sambamba katika maonyesho hayo ili kuwaelimisha na kuwasihi wajasiliamali kujiunga na mfuko huo na kuweza kuwaeleza faida  pindi watakapo jiunga.

Mgeni rasmi aliye hitimisha maonyesho hayo Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Uwekezaji  Dkt. Adelhelm Meru alipata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali ambapo alitembelea banda la PSPF na kuona namnagani wanavyo fanya kazi huku akisifia Mfuko huo kwa kuweza kuanzisha mafao mbalimbali ambayo yanawaokoa wajasiliamali mbalimbali kwa kupata mitaji inayoweza kuwasaidia katika shughuli za kila siku.

Mfuko wa Pesheni wa PSPF ambao unatoa mafao mbalimbali katika jamii likiwemo fao la ujasiliamali, elimu ,uzee ,kifo na mengine mengi umeweza kuendeleza elimu kwa wananchi ili waweze kujiunga na mfuko na kunufaika kwa kutokana na mafao yaliyopo ambapo mtu yeyote anauwezo wa kumudu kwani kupitia mpango wa uchangiaji kw hiari (PSS)  ambao unamwezesha Mwananchi yeyote kuchangia na kunufaika na mafao hayo.

Aidha Afisa Mwendeshaji wa PSPF katika mpango wa uchangiaji wa hiari PSS Haji Jamadary  aliweza kuwaelemisha wananchi mbalimbali walioweza kutembelea banda la PSPF katika maonyesho hayo na kufanikiwa kujiunga na mpango huo wa hiari alisema.

"pindi unapo kuja kujinga na PSS moja kwa moja unakuwa mwanafamiliya Ya PSPF kwani Dhumuni letu ni kukufikia na kukupa huduma zilizo bora na zitakazo kuwa na dhamana katika maisha ya kila mmoja ambapo mwanachama ataweza kunufaika kwa kupata njia ya matibabu kupitia shirika la bima ya afya la taifa NHIF kwani wametia nguvu PSPF ili waweze kuhudumia jamii kwa ujumla Na Kwaharaka zaidi “.

No comments:

Powered by Blogger.