WENGI WAMLILIA MKURUGENZI WA JAMII FORUMS.
Mwanzilishi wa JamiiForums (Mkurugenzi wa Kampuni ya Jamii Media) Maxence Melo, amefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar asubuhi hii.
Anatuhumiwa kwa kushindwa kutoa ushirikiano kwa polisi walipohitaji taarifa za baadhi ya Mtandao wa Jamii Forums.
#FreeMaxenceMelo ndiyo hashi tagi inayosambaa kwa kasi mitandaoni hivi sasa hapa nchini.
Kesi ya Max wa Jamii Forums
Kosa la kwanza: Kuzuia na kuharibu data ambazo Jeshi la Polisi wamekuwa wakitaka kwa ajili ya uchunguzi chini ya kifungu cha 22 cha Cyber Act.
Kosa la Pili: Kushindwa kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi na kuharibu uchunguzi chini ya kifungu 22 cha Cyber Crime
Kosa la Tatu: Kumiliki website ambayo haina domain ya Tanzania (.co.tz) kinyume cha kifungu cha 7 cha sheria ya EPOCA
No comments: