LIVE STREAM ADS

Header Ads

JIMMY GOSPIAN AMJUA MUNGU.



Na George Binagi @BMG
Jimmy Gospian (pichani) ni mwanamziki mpya kwenye muziki wa injili nchini Tanzania. Kabla ya mwaka 2014 alikuwa akifanya muziki wa Bongo Fleva, akiwakilisha mkoa wa Geita na Kanda ya Ziwa kwa ujumla.

Baada ya mwaka 2014, Jimmy Gospian aliamua kugeuza uelekeo na kuanza kuimba nyimbo za injili kwenye matamasha mbalimbali ya injili hususani Kanda ya Ziwa. Baada ya hapo alianza kurekodi albamu yake ambayo hadi sasa jina liko kampuni.

Mwaka huu 2017 ameanza kuachia rasmi baadhi ya nyimbo zilizo kwenye albamu hiyo. Ameanza na wimbo uitwao "Nakujua Bwana" ambao hakika ni wimbo bora kusikiliza na hata mafundisho yake.

"Ni nyimbo nzuri kwa watu wengi hasa wale ambao tunatamani kuisikia faraja ya Bwana ikitenda na sisi. Niwakaribisheni watanzania wote tuisikilize Ninakujua Bwana, ni nyimbo nzuri na natumaini utaifurahia na kuipenda". Amesisitiza Jimmy.
Mwimbaji wa muziki wa injili, Jimmy Gospian (kulia), akizungumza na George Binagi-GB Pazzo wa BMG (kushoto), kuhusiana na ujio wake kwenye muziki huo, baada ya kuachana na muziki wa kidunia.
Sikiliza Mahojiano Hapa kusikiliza mahojiano.

No comments:

Powered by Blogger.