LIVE STREAM ADS

Header Ads

KUHUSU TUKUIO LA MOTO UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA JULIUS NYERERE DAR ES SALAAM.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati), jana akiwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) wakati akitoka kukagua chumba namba cha kuhifadhia mizigo kilichoungua moto jana usiku.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu hatua zilizofikiwa na serikali baada ya kutokea moto huo. Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Gabriel Migile na kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Profesa Ninatubu Lema.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea. 
 Paa la chumba kilichoungua.
 Waandishi wa habari wakiangalia chumba hicho.
 Chumba namba mbili cha kutunzia mizigo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), kikiwa kimetekea kwa moto uliotokea jana usiku katika uwanja huo.
wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

Na Dotto Mwaibale
Serikali imeunda tume ya watu 12 kwa ajili ya kuchunguza tukio la kuungua moto chumba namba mbili cha kuhifadhia mizigo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Akizungumza jana katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa alisema tume hiyo itaongozwa na Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Joseph Nyahende.

"Tume hiyo tumeipa muda wa mwezi mmoja ili kukamilisha uchunguzi huo ambapo tutatoa taarifa kamili ya chanzo cha moto huo" alisema Mbarawa.

Akizungumzia kuhusu tukio hilo alisema moto huo ulitokea jana usiku kwenye chumba namba mbili cha kuhifadhia mizigo ya abiria katika uwanja huo hata hivyo thamani ya vitu vilivyoungua bado haijajulikana.

Katika hatua nyingine Waziri Mbarawa ameinyoonyea kidole kampuni inayofanya kazi ya kupokea mizigo katika uwanja huo ya Swissport kuwa iache kufanya njama za kuzuia kampuni ya Nas Dar Airco iliyopewa mkataba wa kazi katika uwanja kufanya kazi vinginevyo serikali itaifutia leseni.

"Tunataarifa kuwa nyinyi Swissport mnaizuia kampuni hiyo kufanya kazi nasema badilikeni vinginevyo tutawafutia leseni yenu" aliagiza Profesa Mbarawa.

Profesa Mbarawa alitoa maagizo kwa kampuni hiyo ianze kufanya kazi haraka iwezekanavyo kama walivyokubaliana katika mkataba waliopewa.

Mkurugenzi Mkuu wa Swissport Mrisho Yassin hakuweza kuzungumzia suala hilo kwa wakati huo kutokana na mazingira yaliyokuwepo baada ya mkutano huo na alipopigiwa simu baadaye muda wote simu yake ilikuwa ipo bize.
(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

No comments:

Powered by Blogger.