LIVE STREAM ADS

Header Ads

MCHANGO WA TAASISI YA ILTC YA JIJINI MWANZA KATIKA KUKUZA LUGHA MBALIMBALI.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Mwalimu Charles Mombeki ambaye ni Mkurugenzi wa taasisi ya lugha ya International Training Centre (ILTC) iliyopo Isamilo, nyuma ya ofisi za Jiji la Mwanza, alipokuwa akizungumza na 102.5 Lake Fm.
Na BMG
Lugha ni alama muhimu katika jamii yoyote ile. Ni muhimu kwa ajili ya kuwaunganisha watu wa jamii mbalimbali. Bila lugha hakuna mafanikio wala maendeleo katika maisha ya mwanadamu. Inaelezwa kwamba kukanganyikana kwa lugha kulisababisha mafanikio ya ujenzi wa mnara wa Baberi kukwama.

Najua kila mmoja anayo lugha yake ya asili, iwe ya taifa ama kabila. Hoja yangu leo ni juu ya lugha za kukuunganisha na watu mbalimbali kote duniani, kwa ajili ya maendeleo yako. Piga ua, garagaza, hakikisha unajua kuandika na kuzungumza kwa ufasaha lugha ya kiingereza, kwani imekuwa lugha muhimu kote duniani, japo lugha nyingine kama Kiswahili, kifarasa, kichina, kireno, kiitariano, kiarabu na hata lugha yoyote ile, nazo zina umuhimu wake.

Kwa umuhimu huo, BMG inagonga hodi kwenye viunga vya taasisi ya lugha ijulikanayo kama International Language Training Centre (ILTC) iliyopo Isamilo karibu na ofisi za halmashauri ya Jiji la Mwanza. 

Ni baada ya kusikia sifa kede wa kede kuhusiana na taasisi hii, kwamba imekuwa kitovu cha lugha mbalimbali, kuanzia za asili hadi za kimataifa. Nakutana na Mwalimu Charles Mombeki ambaye ni Mkurugenzi wa taasisi hii iliyojizolea sifa lukuki kwa zaidi ya miaka 20.

Mbali na lugha pamoja na masomo ya komputa, taasisi hii pia imeanza kugawa ujuzi kuanzia kwa watoto wadodo, ambapo sasa inatoa masomo ya chekechekea kwa ustadi wa hali ya juu.

Kama hiyo haitoshi, masomo ya ziada ya sayansi na hisabati yanafundishwa katika taasisi hii, ikizingatiwa kwamba hivi sasa wanafunzi wanaosoma masomo hayo, ni lulu kwa Taifa.

Mwalimu Mombeki anasema taasisi yake imejipanga vyema ili kuhakikisha inazalisha matunda bora ikiwa ni hatua za kuunga mkono juhudi za serikali za kuhakikisha taifa linakuwa na wasomi wengi wa masomo ya sayansi.

Inatosha kusema kwamba taasisi ya Internation Language Training Centre ni mkombozi wa lugha kwa watu wote, wawe wanafunzi na hata wasio wanafunzi. Hivyo kwa ukaribu wa Mwalimu Mombeki, fika Isamilo Jijini Mwanza, ili uwe mmoja wa wanufaika wa taasisi hii kwa mwaka huu wa mafanikio wa 2017.

Nami kwa ukaribu wangu, nasema, piga simu nambari 0754 66 49 33 ikiwa unatamani kujiunga na taasisi ya International Language Training Centre. Naitwa George Binagi-GB Pazzo, ahsante kwa kunisikiliza, mfikishie mwenzio ujumbe huu ili naye anufaike.
Bonyeza Hapa Au play hapo chini kusikiliza sauti.

No comments:

Powered by Blogger.