KAMISHNA WA UHAMIAJI MKOANI DAR ES SALAAM ATEMA CHECHE.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Katika hatua nyingine,
Msumule alisema ofisi yake imemkamata raia wa Uganda anayefahamika kwa
jina la Aisha Talib kwa kosa la kuishi bila kibali nchini, pamoja na
kuhodhi pasport 15 za uraia wa Burundi na Madagasc
James Salvatory, Dar
Kamishna wa Idara ya Uhamiaji mkoa wa Dar es Salaam, John Msumule
ametangaza vita kwa watumishi wa serikali hasa wa uhamiaji wanaohusika
na mtandao wa biashara ya utoaji wa vibali vya makazi na vya kazi bandia
kwa raia wa kigeni.
Msumule aliyasema hayo leo
wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amesema kuwa, idara
yake ilifanya ukaguzi katika baadhi ya kampuni, na kukamata hati za
kusafiria bandia zaidi ya 30.
Aidha alitoa
wito kwa waajiri wote kuhakikisha wana ajiri raia wa kigeni wenye vibali
halali vya kazi na makazi, huku akiwataka wageni wasio na vibali kurudi
katika nchi walizotoka.
No comments: