LIVE STREAM ADS

Header Ads

UONGOZI WA UWANJA WA CCM KIRUMBA WATOA SHUKURANI KWA WADAU WA MICHEZO MWANZA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Judith Ferdinand, Mwanza
Uongozi wa Uwanja wa CCM Kirumba unawashukuru   wadau wa michezo   mkoani hapa, waliojitolea kuchangia vifaa vya ujenzi hususani saruji  pamoja na  uchimbaji wa mkondo wa kupitisha maji taka.
 
Hii ni baada ya mkondo huo kuharibiwa na shughuli za kilimo zilizokuwa zinafanyika katika eneo la uwanja huo na kusababisha maji kutuama karibu na lango la kuingilia uwanjani na kuwa kero kwa mashabiki wanaoenda kushuhudia michuano mbalimbali pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi  Kitangiri hasa kipindi cha masika.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Meneja wa Uwanja huo Steven Shija wakati akizungumza na BMG ofisini kwake wilayani Ilemela mkoani Mwanza.

"Tunamshukuru Mungu  na wadau walijitolea kuchangia ujenzi huu wa ukarabati wa mkondo wa kupitisha maji taka, kwani hatua ya awali ya uchimbaji umekamilika kwa asilimia 95   na asilimia 5,  iliyobaki ni mifereji ya  pembeni inayochepukia kwenye mfereji mkuu,  hivyo tunaenda hatua ya ujenzi ambayo imegawanyika katika hatua mbili," alisema Shija.

Shija alisema,hatua ya kwanza ni ujenzi wa daraja na sehemu ya kupokelea maji kuyaelekeza kwenye mkondo mkubwa, hii itasaidia kuzuia maji yasiingie shule ya msingi Kitangiri.

Pia alisema, vifaa  vinavyotakiwa kukamilisha daraja ambalo ndio hatua ya kwanza ya ujenzi huo  ni nondo 20(Mm12),  kokoto tripu 2, mchanga tripu 2, mbao 20(1×8), BRC 6 mita, mawe tripu 4 na  gharama za kulipa mafundi, kwani  kwa sasa wanafunzi na wananchi wanavuka kwa tabu kwenye mtaro huo.

Hata hivyo alisema,hatua ya pili ni kujenga mkondo wa maji sehemu iliyobaki yenye mita 185, ambayo  mahitaji yake  yatatajwa baada ya kukamilisha hatua ya kwanza ambayo ni muhimu  kwa sasa, pia saruji za kuanzia kazi  wanazo.

" Tunaendelea kuamini kuwa kazi hii haitakuwa nyepesi kama wadau hawataweza kujitokeza na kujitolea kwa hali na mali, hivyo tunaomba ushirikiano wenu ili kukamilisha ujenzi huu," alisema Shija.

No comments:

Powered by Blogger.