TAMKO LA OJADACT KUHUSU TUHUMA ZA MAKONDA KUVAMIA STUDIO ZA CLOUDS.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
PRESS CONFERENCE OJADACT MACHI 23, 2017, CCM BUILDING
Maudhui: Uhuru wa Vyombo vya Habari na Usalama wa Vyombo vya Habari.
NDUGU Waandishi wa Habari, Chama cha Waandishi wa Habari wa Kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu Tanzania (OJADACT), leo hii tumewaita hapa kuzungumza nanyi juu ya mwenendo wa Uhuru wa Vyombo vya Habari Nchini na usalama wa Vyombo vya Habari na Waandishi wenyewe.
Waandishi, OJADACT imefuatilia kwa ukaribu tangu litokee sakata la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuvamia kituo cha Clouds media na kubaini mambo mbalimbali , ambayo leo tumeona tuyatolee ufafanuzi zaidi.
Kwanza kabisa, OJADACT tunakili wazi kuwa, hali ya uhuru wa vyombo vya habari Nchini sio nzuri kwa sasa, licha ya kuwepo kwa sheria mbalimbali mbaya hapa Nchini, bado mwendelezo wa kuvinyanyasa vyombo vya habari kupitia wateule wa Rais imeendelea.
OJADACT, tunalaani kitendo hicho kama taasisi nyingine zilivyofanya ,pia kwa ushauri wa vyombo vya habari tunapendekezo yafuatayo;
*Vyombo vya habari vihakikishe vinakuwa na ulinzi wa kutosha kwenye vituo vyao ili kuzuia uvamizi wa watu wasio na nia njema na vyombo vya habari.
*Vyombo vya habari viepuke kuwa na urafiki wa jirani na wanasiasa na viongozi wa Nchi, kwa kuwa, kufanya hivyo kunaweza athiri operesheni za vyombo vya habari pale vinapoonekana kuwakwaza watawala.
*Vyombo vya habari vizingatie sheria ya huduma ya vyombo vya habari ya kuwa na watendaji wenye weledi wa kitaaluma ili kuitendea haki taaluma kwa kutopokea maelezokez
*Vyombo vya habari visiruhusu vyanzo vya taarifa (sources) kuwa sehemu ya kutengeneza maudhui ya habari, wajibu huo waachiwe wahariri wa vyombo vya habari.
*Mahusinao ya vyombo vya habari na wadau yawe na mipaka ili kuepusha mgongano wa maslahi kwenye zoezi la uchakataji wa habari.
*Serikali iheshimu uhuru wa habari hapa Nchini ili vyombo hivyo view chanzo cha kuleta maendeleo.
*Tunampongeza aliyekuwa waziri wetu wa habari Nape kwa maamuzi yake ya kuitetea tasnia.
Edwin Soko
Mwenyekiti, OJADACT
PRESS CONFERENCE OJADACT MACHI 23, 2017, CCM BUILDING
Maudhui: Uhuru wa Vyombo vya Habari na Usalama wa Vyombo vya Habari.
NDUGU Waandishi wa Habari, Chama cha Waandishi wa Habari wa Kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu Tanzania (OJADACT), leo hii tumewaita hapa kuzungumza nanyi juu ya mwenendo wa Uhuru wa Vyombo vya Habari Nchini na usalama wa Vyombo vya Habari na Waandishi wenyewe.
Waandishi, OJADACT imefuatilia kwa ukaribu tangu litokee sakata la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuvamia kituo cha Clouds media na kubaini mambo mbalimbali , ambayo leo tumeona tuyatolee ufafanuzi zaidi.
Kwanza kabisa, OJADACT tunakili wazi kuwa, hali ya uhuru wa vyombo vya habari Nchini sio nzuri kwa sasa, licha ya kuwepo kwa sheria mbalimbali mbaya hapa Nchini, bado mwendelezo wa kuvinyanyasa vyombo vya habari kupitia wateule wa Rais imeendelea.
OJADACT, tunalaani kitendo hicho kama taasisi nyingine zilivyofanya ,pia kwa ushauri wa vyombo vya habari tunapendekezo yafuatayo;
*Vyombo vya habari vihakikishe vinakuwa na ulinzi wa kutosha kwenye vituo vyao ili kuzuia uvamizi wa watu wasio na nia njema na vyombo vya habari.
*Vyombo vya habari viepuke kuwa na urafiki wa jirani na wanasiasa na viongozi wa Nchi, kwa kuwa, kufanya hivyo kunaweza athiri operesheni za vyombo vya habari pale vinapoonekana kuwakwaza watawala.
*Vyombo vya habari vizingatie sheria ya huduma ya vyombo vya habari ya kuwa na watendaji wenye weledi wa kitaaluma ili kuitendea haki taaluma kwa kutopokea maelezokez
*Vyombo vya habari visiruhusu vyanzo vya taarifa (sources) kuwa sehemu ya kutengeneza maudhui ya habari, wajibu huo waachiwe wahariri wa vyombo vya habari.
*Mahusinao ya vyombo vya habari na wadau yawe na mipaka ili kuepusha mgongano wa maslahi kwenye zoezi la uchakataji wa habari.
*Serikali iheshimu uhuru wa habari hapa Nchini ili vyombo hivyo view chanzo cha kuleta maendeleo.
*Tunampongeza aliyekuwa waziri wetu wa habari Nape kwa maamuzi yake ya kuitetea tasnia.
Edwin Soko
Mwenyekiti, OJADACT
No comments: