LIVE STREAM ADS

Header Ads

HALI YA KIELIMU BADO NI CHANGAMOTO MKOANI GEITA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Baadhi ya wadau wa maswala ya Elimu wakiwa kwenye Mkutano wa Takwimu  ya elimu Mkoani Geita.

Wadau wakifuatilia kwa makini taarifa ya utekelezaji sekta ya Elimu Mkoani Geita.

Mratibu wa Marafiki wa Elimu Mkoa wa Geita,Ayubu Bwanamadi ,akitoa taarifa ya tafiti ambazo wamefanya za elimu Mkoani Humo.
Lusenga Manjale akielezea juu ya wazazi na walezi wanavyotakiwa kushiriki katika swala la Elimu.



Mratibu wa Elimu kata ya Buahala hala,Elisha Ngereja akielezea mikakati ya kuboresha Elimu  katika kata zilizopo Mkoani Humo.

Meneja idara ya ushiriki na uajibikaji jamii haki elimu Pius Makomelelo akielezea taarifa ya utekelezaji wa Elimu.


Mwakilishi wa katibu tawala wa Mkoa wa Geita ,Elysalver Nkanga akitoa maelezo kwa wajumbe juu ya ushirikiano na Marafiki wa Elimu Mkoani humo.



Harakati za marafiki wa Elimu,ni muunganiko wa wananchi mmoja mmoja ,makundi na asasi ,taasisi zenye mapenzi na nia ya kuona kunakuwepo maendeleo chanya katika michakato ya utoaji na usimamizi wa elimu  nchini.

Harakati hizo zilianza mwaka 2003 kwa utaratibu wa karibu wa asasi ya hakielimu hadi sasa harakati hizi zina wanachama takribani 40,000 walioenea pande zote za nchi wakiwakirisha makundi mbali mbali ndani  ya jamii ,walimu ,wanafunzi,wanasiasa,wafanyakazi wa umma ,wazazi  na kina mama.

Tangu kuanzishwa kwa harakati hizo marafiki wamekuwa chachu katika uhamsishaji jamii kushiriki katika shughuli za maendeleo ya elimu popote pale walipo.Aidha wamekuwa nyenzo kuu katika kuchangia uwajibikaji wa watendaji na wadau mbali mbali ili kuongeza na kuboresha utoaji wa huduma kwa watu wao.

Ili kuboresha utendaji kazi na ushiriki wa Marafiki katika shughuli za elimu na utawala bora ,Asasi ya HakiElimu kwa kushirikiana na wadau wengine wa Elimu imekuwa ikiwajengea uwezo Marafiki kupitia Mafunzo mbali mbali  na upatikanaji wa taarifa mbali mbali ambazo ni za muhimu katika sekta ya Elimu.

Kutokana na hali hiyo Wadau wa mtandao wa marafiki wa elimu Mkoani Geita,wamekutana na kutoa taarifa ya majumuisho ya ufuatiliaji wa uwajibikaji wa Jamii huku  wakibainisha changamoto kubwa  ambazo wamekutana nazo ni  upungufu wa walimu  kwa baadhi ya shule zina walimu wengi ilihali nyingine zina upungufu mkubwa .Sera ya elimu na Mafunzo imetoa mwongozo  kuwa mwalimu mmoja anatakiwa kuhudumia wanafunzi arobaini na tano.

Akielezea hali ya elimu mratibu wa Marafiki wa Elimu Mkoa wa Geita,Ayubu Bwanamadi alisema tatizo la walimu kuwa wachache ni tatizo kubwa ambalo linaendelea kudidimiza elimu kwani katika darasa nunakuta mwalimu mmoja anafundisha zaidi ya wanafunzi 150 hadi 200 ambapo ni kinyume na sera ya Elimu.


Meneja wa idara ya ushiriki na uwajibikaji jamii Pius Makomelelo ,ametoa mapendekezo ambayo yataboresha elimu ni pamoja viongo kupatiwa elimu ,lakini pia halmashauri  zilizopo Mkoani Hapa kuwekeza kwenye  mafunzo ya Tehama.

Aidha kwa Upande wake Lusenga Robart  Manjale Kutoka Taasisi Ya  CODERT ameelezea masikitiko yake kutokana na hali ilivyo ya mlundikano wa wanafunzi   ambapo alitoa ushauri kwa wazazi na walezi kuchangia swala la elimu na kuacha kusubilia serikali ifanye shughuli hiyo.

Akimwakilisha katibu tawala wa Mkoa wa Geita,Elysalver Nkanga amesema kuwa wataakikisha wanashirikiana na  wadau wa Elimu kuboresha zaidi elimu Mkoani Humo.

IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE.

No comments:

Powered by Blogger.