OJADACT YABAINI CHA ONGEZEKO LA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA NCHINI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Na Nelson Emmanuel,Mwanza
Chama Cha Waandishi wa Habari wa Kupiga Vita Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu Tanzania (OJADACT), kimesema ukosefu wa elimu ya athari za dawa za kulevya kumechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la matumizi ya dawa za kulevya Nchini.
Akiongea mbele ya Waandishi wa habari mapema Jijini Mwanza, Mwenyekiti wa OJADACT, Bwana Edwin Soko, alibainisha kuwa, jamii haina uelewa wa athari za dawa za kulevya hasa kwenye athari na ndio maana vijana wengi wameingia kwenye matumizi ya dawa hizo bila kujitambua.
“ Utakuta mtu anatumia dawa za kulevya kwa dhamira ya kutaka kuonja zinafafanaje na kuamini kesho yake hata tumia dawa za kulevya, lakini kumbe hajui dawa za kulevya hazionjwi” Alisema Bwana Soko.
OJADACT, imesisitiza utoaji wa elimu juu ya dawa za kulevya uzingatiwe na kupewa umuhimu kwenye taasisi za makundi ya vijana kama vyuoni na sehemu za michezo ili kunusuru Taifa kuendelea kuwa na idadi kubwa ya watumiaji wa dawa z akulevya.
Bwana Soko, aliongeza kuwa, kwa sasa OJADACT wamekuwa na kampeni ya kuwahamasisha vijana kwenye mfumo wa kupata elimu juu ya dawa za kulevya kupitia michezo mbalimbali inayoendelea Nchini, kwani michezo ni sehemu ya kujenga afya na kupeana elimu juu ya afya.
Moja ya athari za dawa za kulevya kwa mujibu wa bwana Soko, ni kuathirika kiafya, kimwili na kiroho, ambapo mtu anayepata athari zote hzio uwa ni ngumu sana kukubalika ndani ya jamii, ni wazi sasa jamii lazima ichukue hatua kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya.
Chama Cha Waandishi wa Habari wa Kupiga Vita Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu Tanzania (OJADACT), kimesema ukosefu wa elimu ya athari za dawa za kulevya kumechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la matumizi ya dawa za kulevya Nchini.
Akiongea mbele ya Waandishi wa habari mapema Jijini Mwanza, Mwenyekiti wa OJADACT, Bwana Edwin Soko, alibainisha kuwa, jamii haina uelewa wa athari za dawa za kulevya hasa kwenye athari na ndio maana vijana wengi wameingia kwenye matumizi ya dawa hizo bila kujitambua.
“ Utakuta mtu anatumia dawa za kulevya kwa dhamira ya kutaka kuonja zinafafanaje na kuamini kesho yake hata tumia dawa za kulevya, lakini kumbe hajui dawa za kulevya hazionjwi” Alisema Bwana Soko.
OJADACT, imesisitiza utoaji wa elimu juu ya dawa za kulevya uzingatiwe na kupewa umuhimu kwenye taasisi za makundi ya vijana kama vyuoni na sehemu za michezo ili kunusuru Taifa kuendelea kuwa na idadi kubwa ya watumiaji wa dawa z akulevya.
Bwana Soko, aliongeza kuwa, kwa sasa OJADACT wamekuwa na kampeni ya kuwahamasisha vijana kwenye mfumo wa kupata elimu juu ya dawa za kulevya kupitia michezo mbalimbali inayoendelea Nchini, kwani michezo ni sehemu ya kujenga afya na kupeana elimu juu ya afya.
Moja ya athari za dawa za kulevya kwa mujibu wa bwana Soko, ni kuathirika kiafya, kimwili na kiroho, ambapo mtu anayepata athari zote hzio uwa ni ngumu sana kukubalika ndani ya jamii, ni wazi sasa jamii lazima ichukue hatua kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya.
No comments: