SHIRIKA LA AMANI GIRLS LAWANOA WACHAMBUZI WA SERA JIJINI MWANZA.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Nelson Emmanuel,Mwanza
Shirika la Amani Girls Jijini Mwanza, limeendesha zoezi kwa uchambuzi wa sera mbalimbali Tanzania ili kuweza kuwasaidia watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania wapatiwe huduma bora za afya kwa lengo la kuboresha afya zao.
Wiki hii shirika hilo limefanya uchambuzi wa sera ya vijana kutazama jinsi inavyotoa kipaumbele kwa vijana katika kupata huduma za vitu mbalimbali kama kuwezeshwa kiuchumi, sera ya jinsia wanawake kwa lengo la kutazama vipaumbele na utekelezwaji wa haki za wanawake Nchini.
Naye Mwezeshaji Pentaleon Shoki aliwaeleza washiriki umuhimu wa kupitia sera hizo ni mkubwa, kwani zinawasaidia mabinti kujielewa na kutambua vipaumbele kwa ajili ya kujitambua na kupata haki zao za msingi.
“Tunaweza kuwa na sera nzuri lakini tatizo likawa ni kwenye utekelezaji wa sera hizo na kusababisha jamii kuishi kwenye maisha ya umaskini yanayoweza kuathiri afya zao na kushindwa kuchangia falsafa ya viwanda kwenye kuufikia uchumi wa kati.
Naye Mshiriki wa wa mafunzo hayo Bwana Edwin Soko alisema kuwa, mafunzo hayo ni muhimu kwa vyombo vya habari kushiriki kikamilifu kwenye zoezi la uchambuzi wa sera ili viweze kufikisha ajenda ya haki kwa wanawake mbele ya jamii.
“Vyombo vya habari vina nguvu sana hivyo basi kushirikishwa kwenye chambuzi wa sera ni jambo muhimu kwani vitaweza kusaidia mapambano ya kumpigania mtoto wa kike kwenye kupata haki zao” Alisema Bwana Soko.
Mafunzo hayo yalikuwa ni ya siku moja na kuhusisha wataalamu wa sera takribani ishirini na yalifanyika kwenye hotel ya Adden Palace.
Nelson Emmanuel,Mwanza
Shirika la Amani Girls Jijini Mwanza, limeendesha zoezi kwa uchambuzi wa sera mbalimbali Tanzania ili kuweza kuwasaidia watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania wapatiwe huduma bora za afya kwa lengo la kuboresha afya zao.
Wiki hii shirika hilo limefanya uchambuzi wa sera ya vijana kutazama jinsi inavyotoa kipaumbele kwa vijana katika kupata huduma za vitu mbalimbali kama kuwezeshwa kiuchumi, sera ya jinsia wanawake kwa lengo la kutazama vipaumbele na utekelezwaji wa haki za wanawake Nchini.
Naye Mwezeshaji Pentaleon Shoki aliwaeleza washiriki umuhimu wa kupitia sera hizo ni mkubwa, kwani zinawasaidia mabinti kujielewa na kutambua vipaumbele kwa ajili ya kujitambua na kupata haki zao za msingi.
“Tunaweza kuwa na sera nzuri lakini tatizo likawa ni kwenye utekelezaji wa sera hizo na kusababisha jamii kuishi kwenye maisha ya umaskini yanayoweza kuathiri afya zao na kushindwa kuchangia falsafa ya viwanda kwenye kuufikia uchumi wa kati.
Naye Mshiriki wa wa mafunzo hayo Bwana Edwin Soko alisema kuwa, mafunzo hayo ni muhimu kwa vyombo vya habari kushiriki kikamilifu kwenye zoezi la uchambuzi wa sera ili viweze kufikisha ajenda ya haki kwa wanawake mbele ya jamii.
“Vyombo vya habari vina nguvu sana hivyo basi kushirikishwa kwenye chambuzi wa sera ni jambo muhimu kwani vitaweza kusaidia mapambano ya kumpigania mtoto wa kike kwenye kupata haki zao” Alisema Bwana Soko.
Mafunzo hayo yalikuwa ni ya siku moja na kuhusisha wataalamu wa sera takribani ishirini na yalifanyika kwenye hotel ya Adden Palace.
No comments: