Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Na James bayachamo-Salvanews
Chama cha wanasheria wa Tanganyika (TLS ), kimekabidhi eneo kwa mkandarasi kwa ajiri ya kuanza mara moja kwa ujenzi wa jengo jipya lenye urefu wa ghorofa nne huku likiwa na thamani ya
billion 3.
Akizungumza jana Jijini Dare s salaam wakati wa makabidhiano hayo na mkadarasi , Rais wa chama hicho Tundu Lisu alisema kuwa tangu kuanzishwa kwa chama hicho kimekuwa kikipanga lakini kutokana na jitihada za maraisi waliomtangulia ndyo wamekiwezesha kupata eneo ambalo watajenga na itakuwa ni sehemu ya chama ya kudumu.
Alisema kukamilika kwa jengo hilo linaloanzwa kujengwa may mwaka huu, litakalochukua wiki 56 litawafanya wao kama chama cha wanasheria kuwa na ofisi za kudumu ambayo itawawezesha hata kupangisha baadhi ya watu watakaohitaji kutokana na mahitaji ya wakati huo .
No comments: