Wadau Wa michezo waliojitokeza kusambaza vifusi katika barabara iliopo nje ya uwanja wa CCM Kirumba.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand,Mwanza
Wadau wa michezo kutoka ndani na nje ya Mkoa wa Mwanza, wameombwa kuendelea kushirikiana na uongozi wa uwanja wa CCM Kirumba,ili kuboresha mazingira ya uwanja huo.
Wito huo umetolewa leo na Meneja wa uwanja huo Steven Shija wakati akizungumza na BMG, ofisini kwake jijini Mwanza.
Shija amesema,mazingira ya uwanja yakiwa bora yatasaidia kuendeleza michezo na kuinua uchumi wa mkoa huo,hivyo wadau wanatakiwa kushirikiana ili kufikia lengo.
"Uongozi wa uwanja unaendelea kuwaomba wadau wa michezo ndani na nje ya mkoa wa Mwanza, kuendelea kushirikiana na sisi, ili kuboresha mazingira ya uwanja wetu," amesema Shija.
Pia amewashukuru,wadau waliojitokeza jana kwenye zoezi la kusambaza vifusi vya changarawe katika barabara iliyoharibika nje ya uwanja huo.
Hata hivyo amesema,uongozi Wa uwanja huo unatoa pongezi kwa Mwanza Veterans kujitolea kwa hali na mali kufanikisha upatikanaji wa vifusi vya changarawe pamoja na usambazaji.
Aidha amesema, katika zoezi la usambazaji changarawe wadau mbalimbali walishiriki akiwemo Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Taifa, kutoka Wilaya ya Nyamagana Jamal Abdul Babu,Mwanza Veteran na uongozi wa uwanja.
Judith Ferdinand,Mwanza
Wadau wa michezo kutoka ndani na nje ya Mkoa wa Mwanza, wameombwa kuendelea kushirikiana na uongozi wa uwanja wa CCM Kirumba,ili kuboresha mazingira ya uwanja huo.
Wito huo umetolewa leo na Meneja wa uwanja huo Steven Shija wakati akizungumza na BMG, ofisini kwake jijini Mwanza.
Shija amesema,mazingira ya uwanja yakiwa bora yatasaidia kuendeleza michezo na kuinua uchumi wa mkoa huo,hivyo wadau wanatakiwa kushirikiana ili kufikia lengo.
"Uongozi wa uwanja unaendelea kuwaomba wadau wa michezo ndani na nje ya mkoa wa Mwanza, kuendelea kushirikiana na sisi, ili kuboresha mazingira ya uwanja wetu," amesema Shija.
Pia amewashukuru,wadau waliojitokeza jana kwenye zoezi la kusambaza vifusi vya changarawe katika barabara iliyoharibika nje ya uwanja huo.
Hata hivyo amesema,uongozi Wa uwanja huo unatoa pongezi kwa Mwanza Veterans kujitolea kwa hali na mali kufanikisha upatikanaji wa vifusi vya changarawe pamoja na usambazaji.
Aidha amesema, katika zoezi la usambazaji changarawe wadau mbalimbali walishiriki akiwemo Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Taifa, kutoka Wilaya ya Nyamagana Jamal Abdul Babu,Mwanza Veteran na uongozi wa uwanja.
No comments: