RAMADHANI CUP YAPAMBA MOTO JIJINI MWANZA.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand,Mwanza
Wadau na wapenda michezo mkoani hapa, wametakiwa kushiriki katika mashindano ya ligi ya Ramadhani Cup yaliyoshirikisha timu12 kutoka katika wilaya ya Ilemela na Nyamagana, ambayo yameanza kutimua vumbi hivi karibuni katika uwanja wa Mirongo jijini Mwanza.
Akizungumza jana na BMG Mkurugenzi wa Ramadhani Cup Shafii Said (Chaku),alisema lengo la mashindano hayo ni kuwaepusha vijana katika makundi mabaya hasa katika kipindi hiki cha mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na kukuza na kuendeleza vipaji.
Chaku alisema katika msimu huu wanatarajia kuwepo na upinzani mkubwa kulinganisha na misimu iliyopita kwa sababu timu shiriki zitakuwa na wachezaji tofauti hasa wengi wakitokea ligi kuu kwa kuwa wapo Mwanza kwa ajili ya mapumziko.
Pia alisema timu ambazo tayari zimekwisha jisajiri kushiriki katika mashindano hayo ni Marsh Athlestics, Rumumba Mirror Clane, Uhuru Rangers, Baiko, anaendelea kukamilisha ushiriki wa timu nyingine.
“Mwezi wa Ramadani ni kipindi cha toba nimeandaa mashindano haya, ili kuwasaidia vijana kujiepusha na makundi mabaya ambayo yanaweza kuchoche kufanya dhambi kitu ambacho hakifai kwa kipindi hiki ambapo mpaka sasa ni msimu wa tisa tangu kuanzishwa kwake,"alisema Chaku.
Hata hivyo alisema zawadi ambazo zitatolewa kwa washindi ni mbuzi wawili na kombe kwa mshindi wa kwanza, na mbuzi mmoja kwa mshindi wa pili na zitakuwa na thamani ya sh.950000, amechagua zawadi hizo akiwa na lengo za kutumika kama kitoweo katika siku ya sikukuu ya Eid.
Judith Ferdinand,Mwanza
Wadau na wapenda michezo mkoani hapa, wametakiwa kushiriki katika mashindano ya ligi ya Ramadhani Cup yaliyoshirikisha timu12 kutoka katika wilaya ya Ilemela na Nyamagana, ambayo yameanza kutimua vumbi hivi karibuni katika uwanja wa Mirongo jijini Mwanza.
Akizungumza jana na BMG Mkurugenzi wa Ramadhani Cup Shafii Said (Chaku),alisema lengo la mashindano hayo ni kuwaepusha vijana katika makundi mabaya hasa katika kipindi hiki cha mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na kukuza na kuendeleza vipaji.
Chaku alisema katika msimu huu wanatarajia kuwepo na upinzani mkubwa kulinganisha na misimu iliyopita kwa sababu timu shiriki zitakuwa na wachezaji tofauti hasa wengi wakitokea ligi kuu kwa kuwa wapo Mwanza kwa ajili ya mapumziko.
Pia alisema timu ambazo tayari zimekwisha jisajiri kushiriki katika mashindano hayo ni Marsh Athlestics, Rumumba Mirror Clane, Uhuru Rangers, Baiko, anaendelea kukamilisha ushiriki wa timu nyingine.
“Mwezi wa Ramadani ni kipindi cha toba nimeandaa mashindano haya, ili kuwasaidia vijana kujiepusha na makundi mabaya ambayo yanaweza kuchoche kufanya dhambi kitu ambacho hakifai kwa kipindi hiki ambapo mpaka sasa ni msimu wa tisa tangu kuanzishwa kwake,"alisema Chaku.
Hata hivyo alisema zawadi ambazo zitatolewa kwa washindi ni mbuzi wawili na kombe kwa mshindi wa kwanza, na mbuzi mmoja kwa mshindi wa pili na zitakuwa na thamani ya sh.950000, amechagua zawadi hizo akiwa na lengo za kutumika kama kitoweo katika siku ya sikukuu ya Eid.
No comments: