LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kamati ya Bunge yatua Rock City Mall, kuna jambo imelibaini

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Kamati ya bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa leo imefanya ziara katika jengo la kitega uchumi la Rock City Mall ili kujionea utekelezaji wa mradi huo mkubwa Kanda ya Ziwa.

Na Binagi Media Group
Halmashauri za Jiji la Mwanza pamoja na Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza, zimeendelea na mazungumzo ya namna ya kugawana mrahada wa mradi wa kitega uchumi cha Rock City Mall, baada ya ujenzi wa mradi huo kukamilika.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga ameyasema hayo leo mbele ya kamati ya kudumu ya bunge ya utawala na serikali za mitaa iliyofanya ziara ya kutembelea mradi huo pamoja na miradi ya barabaraba Jijini Mwanza.

Awali kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Jasson Rweikiza ilipongeza ujenzi wa mradi huo, ingawa imesikitishwa ujenzi huo kutowekewa jiwe la msingi wala jengo kuzinduliwa baada ya kukamilika huku wajumbe wengine wakihoji namna mgawanyo wa mrahaba baina ya wabia wa mradi huo ulivyo.

Itakumbukwa kwamba ujenzi wa mradi huo ulianza mwezi Agosti mwaka 2012 baina ya wabia wawili ambao ni mfuko wa pensheni wa LAPF uliyochangia bilioni 74.4 na halmashauri ya Jiji la Mwanza iliyotoa ardhi yenye thamani ya shilingi bilioni 6.16 kabla ya mwaka 2013 Jiji hilo kugawanywa na kuzaliwa halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ulipo mradi huo na hivyo kufanya hadi mradi kukamilika mwezi disemba 2015 wabia kuwa watatu.

Aidha gharama za mradi huo hadi kukamilika kwake ilipaswa kuwa shilingi bilioni 74.4 lakini kutokana na ongezeko la gharama mbalimbali za ujenzi, ujenzi huo uligharibu shilingi bilioni 80.56 huku makubaliano ya mrahaba wa LAPF kuchukua asilimia 60 ya mapato ukiongezeka hadi asilimia 90.

Hatua hiyo ilipelekea mrahaba wa mapato wa asilimia 40 zilizokuwa zikigawanywa kwa halmashauri ya Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela kushuka hadi asilimia 10 hatua ambayo inazirejesha halmashauri hizo kwenye mazungumzo ya namna ya kugawana mrahama huo kwani awali kila halmashauri ilikuwa ikichukua asilimia 20.

Annette Shaoo ambaye ni Meneja wa kampuni ya Mwanza City Commercial Complex Company Limited (MCCCCL) inayosimamia mradi huo, amesema mwezi septemba mwaka huu makusanyo ya kodi yalifikia bilioni 2.9 kwa mwaka na kwamba matarajio ni kufikia bilioni 4.2 kwa mwaka jengo likijaa wapangaji, ingawa kuna changamoto kwa baadhi ya wapangaji kushindwa kulipa kodi ya pango na hatua zimekuwa zikichukuliwa dhidi yao.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa mfuko wa pensheni wa LAPF, Mwanasheria wa mfuo huo Fidelis Mutakyamilwa amesema mapendekezo yaliyotolewa na kamati hiyo ikiwemo kuboresha uendeshaji wa mradi huo yatafanyiwa kazi ili kuvutia zaidi wawekezaji.

Katika kutamatisha ziara hiyo, pia kamati imekagua ujenzi wa barabara ya Tilapia yenye urefu wa mita 600, Uzinza Rufiji mita 167, Isamilo mita 800 ambapo barabara zote zimejengwa kwa kiwango cha lami pamoja na ujenzi wa daraja la Msuka Kilimahewa.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jasson Rweikiza (kushoto) akizungumza wakati kamati yake ilipotembelea mradi wa Rock City Mall. Kulia ni mwanasheria wa mfuko wa pensheni wa LAPF, Adelis Mutakyamilwa
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jasson Rweikiza (kulia) pamoja na Katibu wa kamati hiyo Chacha Nyakega (kushoto)
Mwanasheria wa mfuko wa pensheni wa LAPF, Adelis Mutakyamilwa akifuatilia mjadala wa kamati hiyo
Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mwanne Mchemba akizungumza wakati wa ziara hiyo
Mjumbe wa kamati hiyo, Venance Mwamoto akizungumza baada ya kutembelea mradi wa Rock City Mall
Mjumbe wa kamati hiyo, Zacharia Issaay akizungumza baada ya kutembelea mradi wa Rock City Mall
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga akizungumza kwenye majadiliano hayo
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga (kushoto), Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza (katikati) pamoja na viongozi mbalimbali wakiwa kwenye ziara hiyo

No comments:

Powered by Blogger.