LIVE STREAM ADS

Header Ads

Waziri wa Madini atua Geita, awamu hii kuna jambo lenye ahueni kwa wananchi

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Waziri wa Madini Angellah Kairuki akiwa na Meneja wa Mgodi wa Buckreef mkoani Geita, Peter Zishoo (Katikati) na pembeni ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Geita, Joseph Kasheku Msukuma kwenye ziara ya kutembelea mgodi huo hii leo.
Waziri wa Madini Angellah Kairuki (kushoto) akiwa na mwenyeji wake ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mwl Herman Kapufi (katikati) wakati wa kikao na wabia wa mgodi wa Buckreef kilicholenga kujadili mikakati ya uchimbaji kwenye mgodi huo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita na Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Kasheku Msukuma akiwa kwenye kikao hicho.
Mjiolojia wa mgodi huo, Anthony Minde akisisitiza kutokuafikia kwa suala la kuwalipa fidia baadhi ya wananchi.
Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho

Na Maduka Online
Wizara ya Madini kwa kushirkiana na Wizara ya Ardhi kwa pamoja zinatarajia kufanya upya uhakiki katika mgodi wa Buckreef mkoani Geita ili kuwalipa fidia wananchi wa Kata za Busanda na Kaseme ambao wamekuwa wakidai fidia kwa muda mrefu kwenye mgodi huo.

Hatua hiyo imetokana na kutokuwepo kwa maelewano baina ya wabia wa mgodi huo ambao ni Kampuni ya Tanzam 2000 inayomiliki asilimia 55 huku asilimia 45 zikimilikiwa na shirika la madini nchini (STAMICO) baada ya kushindwa kulipa deni hilo kutokana na kutokuwa na uhakika na madai hayo na kutokuwa na leseni.

Mjiolojia wa mgodi huo, Anthony Minde alisema hakukuwepo mgogoro wowote kwani mkataba wa uthamini ulisainiwa na mkuu wa wilaya pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita wakati huo, hivyo suala la kulipa fidia linakuwa gumu kwa upande wao.

“Nafikiri waliosema kwamba walikuwepo ni kwamba Afisa wa Serikali na ni wa Shinyanga, tuliletewa baada ya kuomba kwamba hii tathmini ifanywe na mtu wa serikali ikaidhinishwa na kusainiwa kwenye ngazi ya wilaya na mkoa kabla ya kuletwa kwetu ili tuisome kuona kama iko sawa, Tunamshangaa Mbunge anaposema ripoti hiyo haikusainiwa” Alisema Minde.
Hata hivyo Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Mkoani Geita Bw Joseph Msukuma aligoma kukubaliana na taarifa hiyo na kudai kuwa walipeleka mthamini ambaye hakuripoti kwenye Halmashauri ya wilaya ya Geita na kwamba walikuwa wakifanya uthamini huku wakiwanyang’anya marudio wananch.

“Walileta mthamini kutoka Shinyanga ambaye hakuripoti kwenye Halmashauri ya wilaya ya Geita, ulipotokea mgogoro pale Kaseme tukaja, mlikuwa mnafanya uthamini mnanyang’anya na marudio ya wananchi, ndo wananchi wakagoma likasimamishwa hilo zoezi, huyo aliyekuja kurudisha kwenye ngazi ya Halmashauri ni nani aliyeridhia? Na kama kweli mlifanya uthamini hawa asilimia mia moja wametokea wapi?” Alisema Msukuma.

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki amechukua uamuzi wa kupeleka madia hayo kwenye wizara ya ardhi na kwamba atamueleza Waziri husika kurudisha wathamini wake kwa mara nyingine ili kujiridhisha kwa kila mwananchi kama anaumiliki halali wa eneo analoliombea fidia.

“Sasa mimi uamuzi wangu ni kwamba, kama Serikali tutakaa tutalipeleka suala hili wizara ya ardhi kupitia kwa waziri wa ardhi ili aelekeze wataalam wake, wathamini wake tena kurudi kwenye jina moja baada ya jingine katika majina hayo elfu moja na sitini na mbili kila mmoja kuweza kujiridhisha eneo lake ni lipi na kama kweli ana umiliki nalo ili baada ya hapo sasa kama wao walikuwa wamesema hawawezi kulipa kwa sababu hawana uhakika na orodha kamili tutakuwa tumelimliza na wasipolipa tutakuwa tumejua nia yao sio nzuri” Alisema Kairuki.

No comments:

Powered by Blogger.