SHULE YA WASICHANA WAJA GEITA YAWAZAWADIA WALIOFANYA VIZURI MASOMO YA SAYANSI KIDATO CHA SITA
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Gari mbili aina ya IST yenye thamani ya shilingi milioni 22 yakiwa yamepakiwa nje ya shule hiyo yakisubiliwa kukabidhiwa kwa wanafunzi hao.
Mwanafunzi ambaye amezwadiwa gari Edina Davis ambaye katika matokeo ya kitaifa alishika nafasi ya Tisa akijaribia gari yake.
Mgeni Rasmi ambaye yupo katika Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Sayansi ,Teknolojia na Ufundi Profesa Simon Msanjila akikata utepe kwaajili ya kuwakabidhi magari wanafunzi hao.
Mwanafunzi Bihera Kabaruka ambaye alikuwa mshindi wa pili kati ya wanafunzi kumi ambao wamefanya vizuri katika mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita.
Mkurugenzi wa Shule binafsi za WAJA zilizopo Mkoani Geita Mhandisi Chacha Wambura akiwakilisha taarifa ya shule hiyo kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Sayansi ,Teknolojia na Ufundi Profesa Simon Msanjila.
Na Joel
Maduka
Mkurugenzi
wa Shule binafsi za WAJA zilizopo Mkoani Geita Mhandisi Chacha Wambura amewazawadia magari mawili
wanafunzi wa kike waliohitumu Kidato cha
Sita katika Shule ya Sekondari ya wasichana WAJA waliotajwa kufanya vizuri
katika masomo ya Sayansii kwenye matokeo ya kidato cha Sita mwaka huu.
Akikabidhi magari
hayo mawili aina ya IST yenye thamani ya shilingi milioni 22, Naibu Katibu Mkuu Wizara
ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Simon Msanjila amewataka wanafunzi wengine kuiga mfano wa
washindi hao na kuzitaka taasisi nyingine pia kuiga mfano uliooneshwa na
Bw.Chacha
Mmoja wa
wanafunzi waliozawadiwa ni Edina Davis ambaye katika matokeo ya kitaifa
alishika nafasi ya Tisa amesema kufanya
kwake vizuri na kupatiwa zawadi ya gari kunatokana na kujituma ili kuipata
zawadi ambayo imekuwa ahadi ya Mkurugenzi wa shule hiyo kwa wanafunzi wote kuwa
angewapatia magari washindi
No comments: