LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAFANYAKAZI WA BIMA YA BRITAM WATOA MSAADA KATIKA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA CHAKUWAMA.

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Mkuu wa operesheni wa Bima ya Britam, Farai Dogo  akikabidhi msaada wa vitu mbalimbali katika kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza jijinini Dar es Salaam ikiwa ni kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza Oktoba duniani Kote.
Meneja masoko wa bima ya Britam,Godfrey mzee akimkabidhi Katibu Mtendaji wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA, Hasan Khamis msaada huo ni shukrani kwa wateja wa bima iyo ambapo wameona watoe faida kwa watoto yatima wanaolelewa katika kituo kilichopo sinza jijini Dar es Salaam.

WAFANYAKAZI wa bima ya Britam ambayo hutoa bima za magari, bima za nyumba, bima za wakandarasi, bima za usafiri wa majini pamoja na bima za safari bima za afya pamoja na nyingine nyingi wametembelea kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza jijini Dar es Salaam.

Wafanyakazi hao wametoa vitu mbalimbali kama vile Unga kilo 300
Maharage 250,Sukari kilo 200,sabuni za unga,Karatasi nyeupe (limu bunda)200,Daftari boksi 500, Mafuta ya kula lita 100,chumvi pamoja na vifaa mbalimbali vya shule.

Vitu hivyo vyote vimegharimu shilingi milioni Saba ambayo wameona wagawane faida waliyoipata katika kushaherekea wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza ya Oktoba duniani kote.

Kwa upandewa  Katibu mtendaji wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA, Hasan Khamis  amewashukuru uongozi kampuni ya bima ya Britam  kwa kuwaona wao kwani kunavituo vingi hapa nchini "Tunashukuru kwa kutuona sisi CHAKUWAMA na kwa kuona mchango wetu.
 Wafanyakazi wa bima ya Britam wakiwa katika picha ya pamoja wakati wakikabidhi vitu mbalimbali kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo sinza jijini Dar es Salaam. 
Katibu mtendaji wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWA, Hasan Khamis akizungumza na wafanyakazi wa bima ya Britam na kuwaelezea historia ya kituo hicho pamoja na changamaoto pamoja na mafanikio waliyoyapata.
Pia amewashukuru wafanyakazi wa bima ya Britam kwa kuwapa msaada huo.
 Baadhi ya wafanyakazi wa bima ya Britam wakimsikili katibu Mtendaji wa kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza jijini Dar es Salaam.
 Wafanyakazi wa Bima ya Britam wakimsikiliza Mlezi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA, Saida Hasan walipotembelea katika kituo chake jijini Dar es Salaam.
 Wafanyakazi wa Bima ya Britam wakiwa katika picha ya pamoja na Mlezi Mkuu wa Kituo cha CHAKUWAMA, Saida Hasan walipotembelea katika kituo chake kilichopo Sinza jijini Dar es Salaam.
 Mfanayakazi wa Bima ya Britam akiwahudumia wateja walipita kupata taarifa mbalimbali za bima hiyo ikiwa ni kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka iki ya kwanza ya mwezi Oktoba.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Bima ya Britam wakiwa katika picha ya  pamoja jijini Dar es Salaam.
Na Michuzi Media Group

No comments:

Powered by Blogger.