WAKAZI WA GEITA WATAKIWA KUWA MAKINI NA MATUMIZI YA MITANDAO
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Naibu mkurugenzi toka mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) Thadayo Ringo akizungumza na waandishi wa habari wakati wa semina ya kuelekezwa namna ya kuhama mtandao bila ya kubadilisha namba ya simu.
Na Maduka Online
Mwandishi mwandamizi wa Nipashe na RFA Mkoani Geita Renatus Masuguriko akiuliza swali wakati wa semina.
Mhandisi mwandamizi Mwesigwa Felician kutoka TCRA akiendelea na semina kwa waandishi wa habari Mkoan Geita.
Mhandisi Mwandamizi Mwesigwa Felician kutoka TCRA akitoa maelekezo kwa wanasemina ambao ni waandishi wa habari Mkoani Geita.
Waandishi wa habari Mkoani Geita wakifuatilia semina kutoka TCRA.
Wananchi Wilayani Geita wametakiwa
kuwa makini pindi wanapotumia mitandao ya simu hasa wakati wa huduma za miamala
ili kuepusha usumbufu utokeao kwa makosa
ya miamala hiyo kwa kuhakiki mara tatu kabla ya kutuma muamala huo.
Wito huo umetolewa na naibu
mkurugenzi toka mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) Thadayo Ringo wakati
wa semina kwa waandishi wa
habari mkoani Geita juu ya huduma ya kuhama toka mtandao mmoja wa simu
kwenda mwingine bila kubadili namba ya simu na kusema kuwa uhahikiki wa muamala
kabla ya kutuma ni muhimu ili kuepuka changamoto za malalamiko ya kupotelewa
fedha.
Akizungumzia faida za huduma ya kuhama toka mtandao
mmoja wa simu kwenda mwingine bila kubadili namba ya simu kwa mteja, mhandisi mwandamizi Mwesigwa
Felicia kutoka TCRA amesema huduma hiyo
inampa nguvu mteja kuchuja huduma bora zaidi toka mtandao mmoja kwenda mwingine
pasipo kuhofika kubadilka kwa namba na
kuongeza ushindani kwenye sekta ya mawasiliano.
No comments: