Kampeni ya "Amsha Kiwanda" kuzinduliwa Jijini Mwanza
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, Mwanza
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella kesho anatarajia kuzindua kampeni ya "Amsha Viwanda" wilayani Nyamagana jijini hapa.
Kampeni hiyo ambayo itafanyika kwa siku tatu kuanzia Novemba 7 hadi 9, katika ukumbi wa Gand Hall jijini hapa, imelenga kuwakutanisha wajasiriamali wachakataji wa bidhaa kwa kuwaunganisha na wadau Wa huduma za kifedha na mamlaka za udhibiti ubora ili waweze kuuza na kusambaza bidhaa zao katika soko la ndani na nje ya nchi.
Hayo yalisemwa jana na Afisa Mradi wa Kusaidia na Kuendeleza Wajasiriamali Tanzania (TLED), Elvis Chuwa kutoka Shirika la Voluntary Service Overseas (VSO), ambao ndio waandaaji wa kampeni ya amsha kiwanda wakishirikiana na SIDO, TCCIA, TWCC na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wakati akizungumza na BMG.
Chuwa alisema, mradi wa kampeni hiyo kwa awamu ya kwanza utafanyika kwa wilaya nne za mkoa wa Mwanza ikiwemo Nyamagana ambayo ndio wanaanzia, Ilemela, Magu na Kwimba ambapo wamelenga kuwafikia wajasiriamali 720, huku wakitarajia 250 kupata nenbo ya ubora na 160 ambao ni wanawake watasajili biashara zao.
"Katika kukamilisha kampeni hiyo kwenye wilaya nne, tunatarajia wanawake wajasiriamali 160 kusajili bidhaa zao,hii ni kutokana na wao kukosa masoko ya bidhaa zao kwa vile wengi wao hawajazisajili, hivyo kupitia hivyo tutakua tumesaidia familia na uchumi wa nchi," alisema Chuwa.
Hata hivyo alisema, kampeni hiyo itawakutanisha wajasiriamali na wadau wa teknolojia ambazo zitawasaidia katika uzalishaji bidhaa kwa urahisi na bora zinazokubalika,pamoja na TBS na TFDA kwa ajili ya kujifunza juu ya ubora wa bidhaa.
Aidha alisema, Amsha Viwanda ni kampeni kwa ajili ya kuwahamasisha wajasiriamali hususani wanawake kwa kuwatangaza na kuunga mkono jitihasa zao kwani wanatambua jitihada na changamoto wanazozipata, hivyo wajitokeze kuhudhiria kwani haina gharama yoyote.
No comments: