Shirika la Under The Same Sun lataka mabadiliko ya sheria kupambana na ukatili kwa wenye ualibino
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma ya Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, Mwanza
Imeelezwa
kuwa kutokana na vitendo vya kikatili vinavyoendelea nchini dhidi ya watu wenye
ualbino, ipo haja ya kufanyia marekebisho baadhi ya sheria hili kunusuru kundi
hilo.
Hii ni
kutokana na kuwepo kwa sheria nchini ambazo hazijaelezea endapo kutatokea mtu
akamfanyia vitendo vya ukatili mtu mwenye ualbino hatua ipi inatakiwa
kuchukuliwa pamoja na adhabu gani inayomstahili kulingana na kosa.
Hayo yalielezwa
jana na Mkurugenzi wa Shirika la Under the Same Sun, Vicky Ntetema katika
warsha ya mpango wa mafunzo ya uhamasishaji wa fursa sawa za ajira na uelewa wa
mifumo ya elimu, sheria za kazi,Haki za binadamu na haki za ajira kwa watu wenye ualbino,
iliyoandaliwa na shirika hilo ambayo
inafanyika kwa siku nne jijini Mwanza.
Ntetema
alisema kuna Sheria nyingi ambazo wao kama watetezi wa haki za binadamu
wangependa zirekebishwe, ikiwemo sheria ya usafirishaji haramu wa viungo vya
binadamu kwa kuongeza vipengele vinavyohusu watu wenye ualbino.
Pia alisema sheria
ya tiba asili na mbadala haielezei vigezo ambavyo mtoa tiba anatakiwa kuwa
navyo ili apatiwe leseni na badala yake inaelekeza vitu anavyotakiwa kutumia
wakati wa kutoa tiba ikiwemo mimea na wanyama ambapo binadamu wapo kundi la
wanyama, hivyo baadhi yao utumia mwanya huo kuwafanyia watu wenye ualbino
vitendo vya kikatili ikiwemo kuwakata nywele zao.
Hivyo
alisema ni wakati wa tume ya haki za binadamu, wanasheria, serikali na wadau
mbalimbali wakutane na kujadili pamoja na kutoa mapendekezo ya takayofanyika
katika kufanyia marekebisho sheria hizo, zinazoonekana kuwapatia mwanya baadhi ya watu ambao siyo
waadilifu ya kuwafanyia vitendo vya kikatili watu wenye ualbino.
Kwa upande
wake Mwanasheria wa Shirika la Under The Same Sun, Maduhu William alisema kuna
haja ya kufanyia marekebisho baadhi ya sheria ambazo zinawanyima fursa za
kupata haki zao za msingi kisheria watu wenye ualbino ikiwemo Sheria ya ndoa ya
mwaka 1971, ambayo aimlazimishi mwanandoa kwenda kutoa ushahidi mahakamani
dhidi ya mwenza wake,hivyo ikitokea baba amemfanyia ukatili mtoto au mtu mwenye ualbino, mama atashindwa kutoa
ushahidi na kupelekea aliyefanyiwa ukatili kutopatiwa haki yake.
Pia alisema
Sheria ya uchawi ya mwaka 1928, Sheria
ya tiba asili na mbadala ya mwaka 2002, Sheria ya ushahidi ya mwaka 2002 na
sheria ya kanuni ya adhabu ni miongoni
mwa sheria zinazotakiwa kufanyiwa marekebisho kulingana na mazingira ili watu
wenye ualbino waweze kuishi kwa amani
sambamba na kukomesha ukatili huo.
Hata hivyo
Maduhu alimuomba Rais John Magufuli asimamie jambo hilo la kufanyia marekebisho
Sheria, I'll haweze kufikia malengo ya kuwa na uchumi wa kati wa viwanda, kwani
hawezi kufanikiwa ikiwa wananchi wake hawataki kutoa nguvu kujishughulisha na
badala yake wamejikita kwenye imani potofu za kuamini kuwa kufanikiwa mpaka
wapate viungo vya watu wenye ualbino.
No comments: