Mshindi wa Rock City Marathon 2017 aweka mambo hadharani
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, Mwanza
Mshindi wa kwanza mashindano ya Rock City Marathon (2017), katika mbio za km tatu maalum kwa ajili ya
wazee, Christina Urio (57) mkazi wa
Mabatini jijini Mwanza, mewataka wazee kujiwekea utaratibu wa kushiriki kwenye mashindano kama hiyo ili kuweka mwili
katika hali kutopata magonjwa.
Mashindano
hayo ambayo yanayoratibiwa na kampuni ya Capital Plus International yalifanyika kwa mara ya nane hivi karibuni
jijini Mwanza ambapo aliibuka mshindi kwa mara ya tano mfululizo katika mbio
hizo.
Hayo
aliyasema jana wakati akizungumza na BMG nyumbani kwake, na kubainisha kwamba
siri ya kushinda nafasi ya kwanza kila mwaka katika mashindano hayo ni kuwa na
utaratibu wa kufanya mazoezi mapema.
Urio alisema
ni vema wazee kutambua umuhimu wa kufanya mazoezi sambamba na kujitokeza kwa wingi katika michezo na mashindano
mbalimbali kama hayo kwani huburudisha na kusaidia kuepusha magonjwa.
Pia alisema
viongozi wanawajibu wa kuwashauri wazee na vijana kufanya mazoezi ili
kuepusha vitendo vya uhalifu, kwani
akili na mawazo yatakuyamejikita kwenye mazoezi na kusahau mambo mabaya hasa
kwa vijana yakiwemo kuvuta bangi kutumia madawa ya kulevya, kuiba na kufanya
mapenzi katika umri mdogo.
Hata hivyo alisema
jamii inapaswa kutambua kuwa michezo
haichagui umri wa mtu kwani kuna baadhi ya watu huwacheka wazee pindi
wanapofanya mazoezi kwa kusema kuwa muda umeshaisha.
“Nasikitika
kuona watu wanawacheka wazee, pindi wanapofanya mazoezi na husau kuwa haya
chagui rika la mtu bali huepusha kupatwa
na magonjwa yasiyo ambukiza kama kisukari na presha,”alisema Urio.
No comments: