Mwanza kuzindua kampeni ya “Furaha Yangu” wikendi hii
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na Judith Ferdinand, BMG
Mkuu wa Mkoa
Mwanza Mhe.John Mongella amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kufanya
vipimo vya Virusi vya Ukimwi, ikiwa ni uzinduzi wa kampeni ya Furaha Yangu ili
kutambua afya zao.
Mhe.Mongella
ametoa rai hiyo leo wakati akizungumza na wanahabari na kubainisha kwamba
kampeni hiyo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi mkoani Mwanza jumamosi Julai 21,
2018 katika uwanja wa Furahisha.
“Nawahimiza
wakazi wa mkoa wa Mwanza hususani wanaume kuungana nami kwenye uzinduzi wa
kampeni hii ili kujua hali ya afya mapema ambapo watakaobainika kuwa na maambukizi
watapata fursa ya kuanza dawa mapema, kupata elimu ili kupunguza uwezekano wa
kuwaambukiza wengine huku wakiishi kwa fuaraha”. Amehimiza Mhe.Mongella
Kwa upande
wake Mganga Mkuu mkoani Mwanza Dkt.Thomas Rutachunzibwa amesema kiwango cha
maambukuzi ya VVU kimepanda kutoka asilimia nne hadi hadi 7.2 hivyo kuna
umuhimu wananchi wakashiriki kwenye kampeni hiyo hatua itakayosaidia kupambana
na kiwango cha maambukizi ya virusi hivyo.
No comments: