RC Mnyeti kuzindua michuano ya Chem Chem Cup 2018
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na Mwandishi Maalum, Manyara
Jumla ya
timu 20, zinatarajiwa kushiriki ligi ya Chem Chem CUP, wilayani Babati mkoa wa
Manyara ambapo zawadi zenye thamani ya sh 4.5 milioni zitatolewa.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Mratibu wa ligi hiyo ambayo hufanyika kila
mwaka,katika uwanja wa Mdori, Charles Godluck alisema, lengo lake ni kupiga
vita ujangili na kuhamamisha jamii
uhifadhi za mazingira.
Godluck
alisema, ligi ya chem chem CUP,mwaka huu inatarajwa kufunguliwa na Mkuu wa mkoa
wa Manyara, Alexander Mnyeti, Agosti 19 na itatanguliwa na mkutano wa kutolewa
jezi wa timu zote agosti 10 mwaka huu.
"hivi
sasa tumezitaka timu zote ifikapo Agosti 4 ziwe zimethibitisha lakini pia
kujitokeza kwenye kikao cha kupanga ratiba Agosti 10"alisema.
Alisema
mwaka huu bingwa wa soka, atapewa zawadi ya fedha taslimu 1.7 milioni na
kombe,mshindi wa pili fedha 1.1 milioni, wa tatu 600.000 na wa nne 300,000.
"pia
kutakuwa na zawadi wa kocha, bora, timu bora na mchezaji bora"alisema
Alisema
katika michuano hiyo, pia kutakuwa na michezo kwa wasichana ambapo, bingwa
atazawadiwa 400,000 na pia kutakuwa na ngoma za kitamaduni na michezo mingine.
Meneja wa
taasisi ya Chemchem Foundation, Recardo Tossi, ambao wamewekeza ujenzi wa
hoteli katika eneo la Mdori, alisema ligi hiyo, imekuwa ikishirikisha zaidi ya
wanamichezi 400 na kuwa na ufanisi mkubwa.
"tunataka
jamii ambayo inazunguka kijiji cha Mdori na tarafa nzima ya Mbugwe na wilaya ya
babati, kuwa wahifadhi wazuri na kupiga vita ujangili"alisema.
Na hapa
chini ni baadhi ya matukio katika picha ya michuano iliyofanyika mwaka jana
ambapo timu ya Mdori fc ilijinyakulia kombe la michuano hiyo.
No comments: