Wafanyabishara watakiwa kuongeza thamani ya madini kabla ya kuyasafirisha
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Naibu Waziri
wa Madini Mhe.Doto Biteko amewataka wafanyabiashara wa madini nchini kufunga
mashine za kukatia madini katika mkoa husika wanaonunua madini kama sheria
inavyoelekeza.
Mhe.Biteko
alitoa kauli hiyo Julai 19,2018 wakati akizungumza na wafanyabiashara wa madini
ya vito katika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma.
Aidha Mhe.Biteko
alisikitishwa na hatua ya baadhi ya wafanyabiashara wanaonunua madini ya vito
ikiwemo Ruby na Gem Stone wilayani Tunduru kutokuwa na mashine za kukatia madini
hayo wilayani humo na badala yake mashine hizo ziko Jijini Dar es salaam.
Alisema
sheria ya uwazi na uwajibikaji katika sekta ya uziduaji, kifungu cha 49 inamtaka
mfanyabishara wa madini anayetoka nje ya nchi kufungua mashine zisizopungua 30 katika
eneo husika analonunulia madini na ikiwa ni mfanyabishara mzawa sharti afunge
mashine zisizopungua tano.
Mhe.Biteko aliongeza
kwamba sheria ya madini ya mwaka 2010 kifungu cha 73 inamtaka wazi kwamba kila
mmiliki wa leseni ya madini (dealer) lazima ayaongeze thamani madini yake kabla
ya kuyasafirisha jambo ambalo linaonekana kukiukwa na wafanyabiashara wengi
nchini.
Kutokana na
hali hiyo, aliwaagiza wafanyabiashara wote nchini kuhakikisha wanatimiza masharti
hayo kwa mujibu wa sheria ndani ya siku 30 baada ya kupewa leseni ambapo
alibainisha kwamba wote walioomba leseni za kufanya biashara ya madini wataanza
kupewa leseni hizo kabla ya mwezi huu kuisha.
Katika hatua
nyingine Mhe.Biteko aliwataka watanzania wanaoingia ubia na wawekezaji kutoka
nje ya nchi kuhakikisha wanaingia makubaliano yanayowanufaisha kwa mjibu wa
sheria badala ya kuingia makubaliano yasiyo na tija kwao ambapo sheria ya
madini inatamka wazi kwamba mwananchi mzawa atakayeingia ubia na mwekezaji
kutoka nje ya nchi anapaswa kupata hisa zisizopungua asilimia 25.
Akisisitiza
kuhusu hilo, Mhe.Biteko alionyesha kukerwa na hatua ya mmoja wa wazee wilayani
Tunduru kuingia ubia na wafanyabiashara wa madini ya vito (Gem Stone) kutoka
nchini Sirilanka huku akiwa hakujui hisa zake katika makubaliano hayo na hivyo
kuonya juu ya makubaliano (mikataba) ya aina hiyo ambayo yanawanyonya wananchi
jambo ambalo serikali haiwezi kulivumilia liendelee.
Naibu Waziri wa Madini Mhe.Doto Biteko akizungumza katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya Tunduru mkoani Ruvuma kabla ya kuanza ziara yake wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya Tunduru Mhe.Juma Homera akitoa taarifa ya upatikanaji madini wilayani humu kwa Naibu Waziri wa Madini Mhe.Doto Biteko.
No comments: