LIVE STREAM ADS

Header Ads

Jeshi la zimamoto mkoani Mwanza latahadharisha ujenzi wa makazi holela

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Judith Ferdinand, BMG
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji  Mkoa wa Mwanza limewatahadharisha wananchi kujiepusha na ujenzi wa makazi katika maeneo hatarishi ikiwemo kwenye miinuko mikali kutokana na usalama mdogo wa maeneo hayo hususani wakati wa majanga.

Kamishina Msaidizi wa Jeshi hilo,  Juma Kwiyamba anasema changamoto zinazowakabili katika utendaji wa kazi ni baadhi ya maeneo kutofikika kirahisi pindi wanapotaka kutoa huduma ya kuzima moto na uokoaji wa watu na mali zao kwani miundombinu  yake siyo rafiki kutokana na ujenzi holela ulifanya na wakazi wa eneo husika  hususani milimani.

Sanjari na hayo alisema, ujenzi holela umesababisha uharibifu wa miindombinu ya maji kwa kuziba au kufukia visima maalum vya maji ya kuzimia moto (fire hydrants), hivyo kupelekea  upatikanaji maji kuwa mgumu wakati wa zoezi la kuzima moto  na kuokoa mali na watu sanjari na   baadhi ya  madereva wa magari yanayotoa huduma tofauti kwa jamii kushindwa kuwapisha  barabarani pindi wanapoku wanaenda kutoa msaada eneo  ilipotokea  dharura ya moto  matokeo yake wanaweza  kusababisha ajali.

Aidha aliwataka wananchi kukata bima za nyumba, hoteli, majengo marefu na vifaa vya moto kama magari ya aina mbalimbali, pikipiki na bajaji ili ajali  ya moto inapotokea wawe wamekidhi vigezo vinavyoitajika na kampuni ya bima husika  ili waweze kupatiwa stahiki zao zinazowahusu pamoja na kuzingatia tahadhari ya moto na kukubaliana na ukaguzi unaofanywa na jeshi hilo.

Alisema jeshi hilo linafanya  ukaguzi kwa lengo la kuboresha na kuimarisha usalama wa raia na mali zao kwenye maeneo husika, kubaini vihatarishi vya moto, kutoa mbinu za kuzuia majanga pamoja na  kukabiliana na moto katika hatua za awali.

"Ni zoezi linalolenga kutoa ushauri wa kitaalum na kisheria kwa umma pamoja na kuweka miundombinu ya tahadhari sanjari na kinga ya kuzuia, kupambana na kuwawezesha watumiaji kujiokoa kirahisi wakati wa dharura", alisema Kwiyamba.
Tamasha la Kinga na Tahadhari dhidi ya Majanga na Moto Jijini Mwanza

No comments:

Powered by Blogger.