Kichocho na Minyoo bado changamoto mkoani Mwanza
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, BMG
Zaidi ya watu milioni 1.5 mkoani Mwanza wanatarajiwa kupata dawa za kinga na tiba ya magonjwa ya kichocho na minyoo ambayo yamekuwa hayapewi kipaumbele, kuanzia Agosti 6 hadi 12 mwaka huu.
Akizungumza jana wakati wa kikao cha utekelezaji mipango ya zoezi la ugawaji dawa hizo, Mratibu wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Mkoa wa Mwanza, Dkt.Mabai Leonard alisema kati ya watu milioni 1.5 wanaotarajiwa kupata dawa hizo, wanafunzi ni 878,624 kutoka shule za msingi 663 huku 627,917 wakiwa ni wanajamii kutoka Kata 41 za halmashauri tano za mkoa zikiwemo Magu,Ukerewe, Buchosa, Sengerema na Jiji la Mwanza.
"Kuna madhara yanayotokana na magonjwa hayo endapo yasipo patiwa kinga na tiba mapema ikiwemo utumbo kujisokota, saratani ya kibofu cha mkojo, ini pamoja na upungufu wa damu na utapia mlo hivyo ni fursa kwa wananchi kujitokeza katika kampeni zoezi hili”. Alisema Dkt.Mabai na kuongeza;
“Katika tathimini ya awali iliyofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Tanzania (NIMR), mkoa wa Mwanza una asilimia 81 ya watu wana maambukizi ya kichocho na minyoo hivyo Serikali imekuja na kampeni ya kutoa chanjo ya magonjwa hayo ili kuyadhibiti”. Alibainisha.
Naye Afisa Mpango wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Oscar Kaitaba alisema zoezi hilo litafanyika kuanzia ngazi ya shule ambapo itawahusu watoto wenye umri kuanzia miaka mitano hadi 14 kwa siku moja ya Agosti 6 na wanafunzi watapatiwa ya Praziquantel kwa ajili ya kichocho na Albendazole ya minyoo kwa ajili ya kukinga na kutibu.
Alisema kwa upande wa jamii watagawa dawa aina moja ya Praziquantel kwa ajili ya kichocho kwa watu wenye umri wa miaka mitano na kuendelea pamoja na kuwashauri kwenda hospitali kupima ili wapatiwe dawa za minyoo na kuzingatia usafi ili kujiepusha na magonjwa hayo.
Naye Mganga Mkuu wilayani Ilemela, Dkt.Florian Tinuga alisema kwenye kampeni hiyo wanatarajia kuwapatia dawa wanafunzi 96,200 waliopo shule za msingi huku ngazi ya jamii hawata husika kutokana na mwezi Februari mwaka huu NIMR walitoa dawa katika maeneo ya ukanda wa Ziwa Victoria katika wilaya hiyo.
Judith Ferdinand, BMG
Zaidi ya watu milioni 1.5 mkoani Mwanza wanatarajiwa kupata dawa za kinga na tiba ya magonjwa ya kichocho na minyoo ambayo yamekuwa hayapewi kipaumbele, kuanzia Agosti 6 hadi 12 mwaka huu.
Akizungumza jana wakati wa kikao cha utekelezaji mipango ya zoezi la ugawaji dawa hizo, Mratibu wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Mkoa wa Mwanza, Dkt.Mabai Leonard alisema kati ya watu milioni 1.5 wanaotarajiwa kupata dawa hizo, wanafunzi ni 878,624 kutoka shule za msingi 663 huku 627,917 wakiwa ni wanajamii kutoka Kata 41 za halmashauri tano za mkoa zikiwemo Magu,Ukerewe, Buchosa, Sengerema na Jiji la Mwanza.
"Kuna madhara yanayotokana na magonjwa hayo endapo yasipo patiwa kinga na tiba mapema ikiwemo utumbo kujisokota, saratani ya kibofu cha mkojo, ini pamoja na upungufu wa damu na utapia mlo hivyo ni fursa kwa wananchi kujitokeza katika kampeni zoezi hili”. Alisema Dkt.Mabai na kuongeza;
“Katika tathimini ya awali iliyofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Tanzania (NIMR), mkoa wa Mwanza una asilimia 81 ya watu wana maambukizi ya kichocho na minyoo hivyo Serikali imekuja na kampeni ya kutoa chanjo ya magonjwa hayo ili kuyadhibiti”. Alibainisha.
Naye Afisa Mpango wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Oscar Kaitaba alisema zoezi hilo litafanyika kuanzia ngazi ya shule ambapo itawahusu watoto wenye umri kuanzia miaka mitano hadi 14 kwa siku moja ya Agosti 6 na wanafunzi watapatiwa ya Praziquantel kwa ajili ya kichocho na Albendazole ya minyoo kwa ajili ya kukinga na kutibu.
Alisema kwa upande wa jamii watagawa dawa aina moja ya Praziquantel kwa ajili ya kichocho kwa watu wenye umri wa miaka mitano na kuendelea pamoja na kuwashauri kwenda hospitali kupima ili wapatiwe dawa za minyoo na kuzingatia usafi ili kujiepusha na magonjwa hayo.
Naye Mganga Mkuu wilayani Ilemela, Dkt.Florian Tinuga alisema kwenye kampeni hiyo wanatarajia kuwapatia dawa wanafunzi 96,200 waliopo shule za msingi huku ngazi ya jamii hawata husika kutokana na mwezi Februari mwaka huu NIMR walitoa dawa katika maeneo ya ukanda wa Ziwa Victoria katika wilaya hiyo.
No comments: