Michuano ya Lake Zone Pre-Season Tournament kutimua vumbi mwezi huu Jijini Mwanza
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, BMG
Mashindano
ya Lake Zone Pre-Season Tournament mwaka 2018 yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi
Agosti 04 hadi 15 katika uwanja mkongwe na wa kisasa wa Nyamagana Jijini
Mwanza.
Mwakilishi
wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano
hayo, Cuthbert Japhet anasema yamelenga kuzipa
nafasi timu za Kanda ya Ziwa kujiandaa na ligi za kitaifa ikiwemo daraja la
kwanza, la pili na ligi kuu kwa msimu huu kwani timu nyingi hazipati nafasi ya
kucheza mechi za kirafiki.
Japhet anasema
mashindano hayo yameandaliwa na
Cleverland Company Ltd wakishirikiana na Chama cha Soka Mkoa wa Mwanza
(MZFA) na mpaka sasa timu nne zimethibitisha kushiriki ikiwemo Mbao FC ambayo ndio wenyeji, Mwadui
FC, Kagera Sugar na GPCO huku wakiendelea kufanya mazungumzo na baadhi ya timu
kama Biashara FC na Singida United.
Anasema kila
timu zitacheza michezo mitatu na mshindi atapatikana kwa atakayekuwa na pointi
nyingi ambapo atapatiwa kikombe na
wapili atapata medali huku sehemu mapato yatakayo patikana wakipelekwa kama msaada
katika kituo cha watoto wenye ualbino cha Mtindo na cha Wazee Bukumbi.
Naye
mwakilishi wa MZFA, Erastus Mayala anawahimiza wadau wa soka kujitokeza kwa
wingi kwenye mashindano huku akisema hiyo ni fursa nzuri kwa timu shiriki
kujiandaa kuelekea msimu wa ligi kuu Tanzania
Bara pamoja na ligi mbalimbali.
No comments: