Mkuu wa Mkoa Mwanza afanya mazungumzo na Kamanda mpya wa jeshi la Polisi
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa
Mwanza Mhe. John Mongella (katikati) leo amekutana na kufanya mazungumzo mafuki na Kamanda
mpya wa jeshi la polisi mkoani hapa, ACP. Jonathana Shanna (kulia) aliyefika ofisini
kwake kujitambulisha.
Pia Mhe.
Mongella ametumia fursa hiyo kuagana na aliyekuwa Kamanda wa polisi mkoani
Mwanza DCP. Ahmed Msangi (kushoto) ambaye amehamishiwa Makao Makuu ya jeshi hilo jijini
Dar es salaam ambapo mazungumzo yao yamejikita katika kuendelea kuimarisha hali
ya ulinzi na usalama mkoani Mwanza.
Mapema
asubuhi ACP. Shanna akizungumza na maafisa wa jeshi la polisi mkoani Mwanza,
alionya kuhusu vitendo vya uhalifu na kuahidi kuvitokomeza ambapo DCP. Msangi
aliwasihi maafisa hao kumpa ushirikiano wa kutoka kama waliokuwa wakimpa ili
kutimiza vyema majukumu yake.
No comments: