Mwanza watakiwa kuzingatia matumizi bora ya vyoo
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, BMG
Wananchi
mkoani Mwanza wametakiwa kuendeleza utamaduni wa kujenga na kutumia vyoo bora
ili kuepukana na maambukizi ya magonjwa ya kuhara yanatokanayo na minyoo ama
kichocho.
Mratibu wa magonjwa
yaliyokuwa hayapewei kipaumbele, Dkt.Mabai Leonard ametoa rai hiyo wakati
akizungumza na wanahabari na kuongeza kwamba magonjwa ya minyoo na kichocho
yanaweza kuambukizwa ikiwa wanajamii hawatazingatia usafi ikiwemo kujisaidia
ovyo badala ya kutumia vyoo.
Alisema
ugawaji wa dawa pekee hauwezi kumaliza magonjwa hayo hivyo ni vyema jamii
ikahakikisha inazingatia kanuni za usafi, kunawa mikono baada ya kutoka chooni,
kunawa vyema kabla na baada ya kula pamoja na kuzingatia usafi wa mwili na
mazingira.
Na
Dkt.Rehman Maggid kutoka mpango wa taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa
hayapewi kipaumbele alisema zoezi la ugawaji dawa katika ngazi ya jamii
linaendelea tangu Agosti 06 hadi 12, 2018 hivyo jamii inapaswa kuhamasika
kutumia dawa hizo.
No comments: