LIVE STREAM ADS

Header Ads

Tambo za Alliance na Mbao kuelekea kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Judith Ferdinand, BMG
Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara msimu wa mwaka 2018/19 unaanza rasmi kutimua vumbi hii leo Agosti 22, 2018 ambapo kwa Jiji la Mwanza mashabiki wanatarajia kushuhudia soka la ushindani baina ya timu za Alliance FC na Mbao FC katika uwanja wa CCM.

Kocha wa timu ya Alliance FC, Mbwana Makata anasema maandalizi yanaendelea vyema na kikosi chake kimejipanga kuhakikisha kinaibuka na ushindi kwenye mchezo huo licha ya kwamba ni mara yao ya kwanza kushiriki ligi hiyo.

"Matumaini ya kupata ushindi ni makubwa katika mechi ya ufunguzi dhidi ya majirani zetu Mbao FC kwani tumejiandaa kwa kucheza michezo mingi ya kirafiki na timu ambazo zina uzoefu katika ligi kuu ikiwemo Kagera Sugar, Singida United, Stend United na Biashara FC hivyo zimetufanya tujiamini" Alisema Makata.

Alisema wachezaji wake wawili Jamal Sudi na Juhudi Samweli wataukosa mchezo huo wa ufunguzi kutokana na kushtuka nyama za paja licha ya kwamba hali zao zinaendelea vizuri japo bado wapo katika matibabu.

Nahodha wa Alliance FC, Hance Masoud alisema wamejiandaa vyema na wachezaji wana morali ya kufanya vizuri hivyo mashabiki wa timu hiyo wajitokeze kwa wingi kuishangilia timu yao kwenye michezo yote.

Naye Kocha wa Mbao FC, Amri Said alisema anajivunia timu timu hiyo na anamatumaini makubwa ya kufanya vizuri katika mchezo huo na ligi kwa ujumla na kwamba kikosi kipo kamili  kwani wamecheza mechi nyingi za kirafiki kwa ajili ya kujiandaa.

Aliwapongeza mashabiki kwa mshikamano waliouonyesha msimu uliopita hivyo aliwaomba kuendelea kuiunga mkono timu hiyo ili iweze kufanya vizuri katika msimu.

No comments:

Powered by Blogger.