Baada ya uzinduzi wa Tuliza Mawimbi, mikakati ya Ebenezer Family Band hii hapa
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, BMG
Kwaya ya muziki
wa injili ya “Ebenezer Family Band” ya Jijini Mwanza imekusudia kufanya harambee
na matamasha mbalimbali ndani na nje ya mkoa wa Mwanza ili kuhakikisha
zinapatikana fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha kulelea watoto wanaoishi
katika mazingira magumu.
Msemaji wa
kwaya hiyo kutoka kanisa la EAGT Kiloleli chini ya Mchungaji Dkt. Jacob
Mutashi, Fabian Fanuel ambaye pia ni Mkurugenzi wa kampuni ya kuchipua na
kuendeleza vipaji ya Famara Promotions aliyasema hayo jumapili iliyopita kwenye
uzinduzi wa albamu ya Tuliza Mawimbi ambapo alisema zinahitajika shilingi
milioni 500 ili kukamilisha ujenzi huo.
Alisema
kwenye uzinduzi wa albamu hiyo kiasi cha shilingi milioni 100 kilipatikana na
kwamba mikakati mingine ya kwaya hiyo ni kufungua studio ya kisasa kwa ajili ya
muziki na video.
“Baada ya
uzinduzi wa leo tunatarajia kuelekeza nguvu katika mikoa ya Geita, Shinyanga,
Simiyu, Mara, Kagera, Kigoma, Tabora kabla ya kuelekea katika mikoa mbalimbali
nchini”. Alisema Fanuel.
No comments: