Kirumba hiyooo fainali ya Angeline Jimbo Cup 2018
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, BMG
Timu ya Kata
ya Ibungilo na Kirumba imefanikiwa kufuzu kuingia fainali katika mashindano ya
Angeline Jimbo Cup msimu wa 2018/19.
Katika
fainali hiyo ambayo inachezwa kesho Septemba 17, 2018 katika uwanja wa CCM Kirumba
huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Naibu
Waziri Sera, Bunge, Kazi, Vijana,Ajira na Walemavu Athony Mavunde.
Kirumba
imefuzu kuingia fainali baada ya kuichapa Nyakato goli 1-0 mchezo uliochezwa
kwenye uwanja wa sabasaba kupitia mshambuliaji wake Baraka David dakika ya 66 huku Ibungilo
ikifanikiwa kuilaza chali Kawekamo kwa kufunga goli 1-0 kupitia Tete Jadwa.
Akizungumza
na BMG, Kocha wa timu ya Ibungilo Swala Daud alisema, anamshukuru Mungu hadi
kufikia fainali na Chapili ni Mbunge
Angelina Mabula kwa kuanda michuano hiyo pamoja na mashabiki wa timu hiyo kwa ushirikiano
walioonesha.
Pia alisema
mchezo wa fainali ni mgumu lakini wao wamejianda kushinda kwani wanaamini Kirumba
watakuwa na lengo la kulipiza kisasi baada ya kuwafunga katika mechi ya ufunguzi.
Mshindi wa
kwanza katika mashindano hayo atajinyakulia
kitita cha milioni 2, kombe, mpira mmoja pamoja na seti moja ya jezi,
mshindi wa pili ataondoka na milioni
1.5, kombe, jezi seti moja na mpira
mmoja huku wa tatu akipata milioni 1, kombe, mpira pamoja na jezi seti moja.
No comments: