Malengo ya wana Bujora kupata shule ya sekondari yatimia
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
SOMA>>>Zahanati ya John Mongella yarahisisha huduma za afya kwa wananchi
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Ujenzi wa
shule ya sekondari ya Kata ya Bujora wilaya Magu mkoani Mwanza unaendelea vyema
na mwakani shule hiyo itaanza kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza.
Mkurugenzi
wa halmashauri ya wilaya Magu, Lutengano Mwalwiba anasema ujenzi huo umetokana
na jitihada za wananchi wa Kata hiyo kwa kushirikiana na viongozi mbalimbali ili
kuhakikisha Kata hiyo mpya inapata shule baada ya kugawanywa kutoka Kata ya
Kisesa na tayari imepata nambari ya usajili.
Jana Wajumbe
wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT) tawi la Mkoa wa Mwanza
walitembelea shule hiyo na kuridhishwa na ujenzi wake ambapo kukamilika kwake kutatoa
fursa kielimu kwa wanafunzi wa Kata ya Bujora.
Ujenzi wa jengo la maabara za masomo ya "Bilogy, Chemistry na Physics" shule ya sekondari Bujora
SOMA>>>Zahanati ya John Mongella yarahisisha huduma za afya kwa wananchi
No comments: