OSHA kuanzisha Oparesheni Maalum kwa waajiri wote nchini
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Wakala wa usalama
mahala pa kazi nchini OSHA unatarajia kuanzisha oparesheni maalum kwa waajiri
wote ili kuhakikisha ikiwa wamejisajili na wakala huo kama ilivyo matakwa ya
kisheria.
Kaimu
Mtendaji Mkuu OSHA, Khadija Mwenda ameyasema hayo hii leo kwenye semina/ kikao
kazi na wanahabari mkoani Mwanza, kilichofanyika katika ukumbi wa Nyakahoja.
Amesema
katika kuboresha mazingira ya ufanyaji kazi nchini, OSHA imeondoa gharama za
ujali kwa kila mwajiri lakini bado mwitikio kwa waajiri kujisajili bado ni
mdogo hivyo wakala huo umepanga kuanza oparesheni maalum kuanzia mwezi huu hadi
Disemba ili kuhakikisha kila mwajiri anasajiliwa.
Mwenda
amesema ikiwa mwajiri atakutwa hajajisajili OSHA hatua za kisheria zitachukuliwa
dhidi yake hivyo waajiri wote wahakikishe wanasajiliwa kabla oparesheni hiyo
haijawafikia kwani kujisajili ni bure.
“Kwa kipindi
hiki cha kuanzia mwezi huu Septemba mpaka Disemba, tutaendesha oparesheni
maalum katika Kanda zetu sita ambazo ni Kanda ya Ziwa, Nyanda za Juu Kusini, Pwani,
Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kusini na Kanda ya Kati na tutapita kila eneo la
kazi kuhakikisha waajiri wamejisajili na kupata cheti cha kukidhi viwango vya
usalama”. Amesema Mwenda.
Baadhi ya
wanahabari walioshiriki semina/ kikao kazi hicho wameahidi kuitumia vyema elimu
waliyoipata kwa kuwaelimisha waajiri na waajiriwa ili kutambua umuhimu wa
kuzingatia usalama mahala pa kazi pamoja na kujisajili OSHA.
Takwimu za
shirika la kazi duniani ILO zinaonyesha kwamba kila baada ya sekunde 15 mfanyakazi
mmoja hupoteza maisha kutokana na ajali ama ugonjwa mahala pa kazi huku
wafanyakazi 160 wakipata ajali.
Aidha
takwimu hizo zinaonyesha kwamba zaidi ya watu Milioni mbili huumia katika
maeneo yao ya kazi kila mwaka na hivyo kusababisha gharama kubwa ikiwemo za
matibabu, fidia, ulemavu, vifo na matengenezo ya mitambo sababu kubwa ikiwa ni
ukosefu wa usalama mahala pa kazi.
Kaimu Mtendaji Mkuu OSHA, Khadija Mwenda akizungumza kwenye kikao kazi hicho
Mwezeshaji wa semina hiyo, Mjawa Mohamed kutoka OSHA akifafanua jambo
Mwanahabari Mashaka Batazar akichangia mada
Mwanahabari Alex Sanga akichangia mada
Mwanahabari Alex Gwido akichangia mada
Washiriki wakiteta jambo kwenye semina hiyo
Tazama BMG Online Tv hapa chini
No comments: