Kaimu Sheikh Mkoani Mwanza aeleza vipaumbele vyake kuifikia BAKWATA Mpya
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Kaimu Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza, Sheikhe Hassan Kabeke akiweka saini kwenye kitabu cha wageni kwenye
ofisi za baraza hilo, kwenye hafla ya kumpokea rasmi tangu ateuliwe kushika
nafasi hiyo. Wanaoshudia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Baraza hilo, Amran
Batenga, aliyekuwa akikaumu nafasi hiyo, Hamis Almas pamoja na Kaimu Katibu wa
baraza hilo, Sina Mwagalazi.
Kaimu Sheikhe mkoani Mwanza, Sheikhe Hassan Kabeke (kushoto) akiteta jambo na mtangulizi wake, Sheikhe Hamis Almas (kulia) muda mfupi baada ya kumvisha joho.
Kaimu Sheikhe mkoani Mwanza, Sheikh Hassan Kabeke akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya
BAKWATA Mwanza, Masheikhe wa Wilaya, Kata na Misikiti ya Wilaya zote za Mkoa wa
Mwanza.
Kaimu Sheikhe mkoani Mwanza, Sheikh Hassan Kabeke akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya
BAKWATA Mwanza, Masheikhe wa Wilaya, Kata na Misikiti ya Wilaya zote za Mkoa wa
Mwanza. Picha na Baltazar Mashaka
Judith Ferdinand, BMG
Baraza la
Waislamu (BAKWATA) Mkoa wa Mwanza limedhamiria kuwaunganisha watanzania wote
ili kuendeleza umoja, mshikamano na amani katika nchini.
Kaimu Sheikhe
mkoani Mwanza, Sheikhe Hassan Kabeke aliyasema hayo Oktoba 24, 2018 wakati
akizungumza kwenye hafla ya kumpokea rasmi tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo
hivi karibuni.
Sheikhe
Kabeke ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini
mkoani Mwanza, alisema katika ungozi wake ataanza kwa kuwaunganisha pamoja waislamu
ili wawe kitu kimoja na kutatua migogoro iliyokuwa inawasibu pamoja pamoja na watanzania
kwa ujumla bila kujali itikadi zao kwa ajili ya maendeleo na amani ya nchi.
Alisema atahakikisha
anajenga nguzo za kiuchumi ndani ya baraza hilo kwa kudhibiti vyanzo vya mapato
vilivyopo na kubuni vyanzo vipya.
Aidha
aliahidi kuimarisha mafunzo ya dini hiyo kwa kuboresha madrasa katika maeneo ya
misikiti na kwamba hayo yatafanyika kwa kasi kubwa ili kuunga mkono kauli ya
Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikhe Abubakary Zubeir ya kuwa na BAKWATA Mpya.
Kwa upande
wake Naibu Mwenyekiti wa BAKWATA (akina mama) Wilaya ya Ilemela Bakwata, Hajida
Omary alisema wamefarijika kumpata Kaimu Sheikh Mkoa wa Mwanza na kuahidi
ushirikiano katika kuwaunganisha waislamu wote.
Naye Katibu
wa Msikiti wa Raudawa ambaye ni pia Mjumbe wa BAKWATA Halmashauri ya Mkoa Mwanza,
Sheikhe Abdalah Khan alisema wapo tayari kushirikiana na Kaimu Sheikh mkoa
Mwanza huku akiwataka waislamu kwa pamoja washirikiane ili waweze kufikia
malengo ya Mufti Mkuu nchini ya kuwaleta pamoja waumini wa dini hiyo.
No comments: