Mtendaji Mkuu NFRA aridhishwa na ubora wa nafaka mkoani Ruvuma
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Kaimu Afisa
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Bi.Vumilia
Zikankuba (katikati) akikagua mahindi wakati wa ununuzi katika kituo cha ununuzi cha
Kigonsela kilichopo mkoani Ruvuma.
Kaimu Afisa
Mtendaji NFRA Bi.Vumilia Zikankuba (wa tano kushoto) akisisitiza jambo baada ya kutembelea kituo cha ununuzi cha Kigonsela mkoani koani
Ruvuma.
Afisa ubora
wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), akikagua mahindi kwenye kituo
cha ununuzi cha Kigonsela mkoani Ruvuma.
Na Mathias Canal, NFRA
Zoezi la
kununua nafaka ya mahindi kwa ajili ya akiba ya taifa ya chakula linaendelea
katika maeneo mbalimbali nchini ambapo wakulima kwa kiasi kikubwa wameitikia
wito uliotolewa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) wa kutonunua
mahindi yasiyokuwa na ubora.
Hata hivyo
baadhi ya maeneo kumeibuka changamoto ya ubora wa mahindi kutokana na
changamoto ya mvua za msimu pamoja na jua kali hali iliyosababisha mazao
kuharibikia shambani.
Kaimu Afisa
Mtendaji Mkuu NFRA), Bi.Vumilia Zikankuba ameendelea na ziara ya kikazi ya
kutembelea vituo mbalimbali vya ununuzi ambapo hivi ambapo Oktoba Mosi, 2018 alitembelea
kituo cha ununuzi cha Kigonsela kilichopo mkoani Ruvuma kukagua mwenendo wa
zoezi la ununuzi katika kituo hicho.
Katika ziara
hiyo ya Mtendaji Mkuu wa NFRA mkoani Ruvuma ambaye pia ni Meneja wa Kanda ya
Songea, Amos Mtafya alieleza kuwa Kanda ya Songea pekee imepangiwa kununua
jumla ya tani 7, 000 kwa awamu ya kwanza ya ununuzi na hadi kufikia jana, Kanda
hiyo ilikuwa imenunua zaidi ya tani 6,000.
Ili
kuimarisha dhana ya Ushirika, Wakala umenunua kwa kiasi kikubwa mahindi kupitia
vyama ya Ushirika na vikundi vya wakulima yaani SACCOS na AMCOS ambazo jumla
yake ni 23 zilizobainishwa na uongozi wa Mkoa Ruvuma.
Vikundi
hivyo vya wakulima ni kutoka katika Halmashauri ya Wilaya Madaba, Songea
Vijijini, Mbinga Mji, Mbinga Vijijini,
Namtumbo na Wilaya Nyasa.
Bi. Zikankuba
aliridhishwa na hali ya ubora wa nafaka iliyonunuliwa na kuwahimiza watumishi
wa NFRA kuendekea kusisitiza na kununua mahindi yenye vigezo vya ubora unaokubalika
kwa ajili ya Hifadhi ya Taifa ya Chakula.
Katika hatua
nyingine Bi. Zikankuba aliwapongeza watumishi wa NFRA kwa kazi nzuri ya wanayoifanya
katika kutekeleza majukumu yao na wakala kwa ujumla.
No comments: