LIVE STREAM ADS

Header Ads

Naibu Waziri Nyongo akagua migodi ya makaa ya mawe mkoani Songwe

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Meneja Migodi kutoka Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Alphonce  Bikulamchi (katikati) akielezea shughuli za uchimbaji  wa makaa ya mawe zinavyofanyika katika Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kabulo uliopo katika mkoa wa Songwe kwa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kushoto). 
Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira uliopo katika wilaya ya Ileje Mkoani Mbeya,  Samwel Kibaranga (kushoto) akimwonesha Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa pili kushoto) reli inayotumika kwa ajili ya kusafirisha makaa ya mawe (haionekani pichani).
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa tatu kushoto mbele) akitoa maelekezo katika eneo la Mgodi wa Mkaa ya Mawe wa Kiwira.
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa tano kushoto mbele) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira mara baada ya kumalizika kwa mkutano.

Na Greyson Mwase
Tarehe 19 Oktoba, 2018 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo alifanya ziara katika Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kabulo (Kabulo Coal Mine) uliopo katika eneo la Kabulo lililopo katika wilaya Songwe mkoani Songwe na Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira (Kiwira Coal Mine) iliopo katika Wilaya ya Ileje mkoani Mbeya.

Baada ya kufanya ziara katika migodi husika, alizungumza na wafanyakazi wa Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira lengo likiwa ni kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Akizungumza katika mkutano wa wafanyakazi alisema kuwa, kwa sasa Serikali imetenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa barabara ya kutoka Kabulo hadi Kiwira itakayotumika kwa ajili ya usafirishaji wa makaa ya mawe pamoja na kuhakikisha inalipa stahili za wafanyakazi mara baada ya taratibu kukamilika.

Katika hatua nyingine, Nyongo aliwataka watumishi kufanya kazi kwa ubunifu na kusisitiza kuwa Wizara ya Madini itahakikisha wanafanya kazi katika mazingira mazuri.

Wafanyakazi wa Mgodi wa Kiwira walimpongeza Naibu Waziri Nyongo kwa kazi kubwa ya kusikiliza na kutatua kero za wachimbaji wa madini nchini pamoja na Taasisi zilizopo chini ya Wizara.

No comments:

Powered by Blogger.