Benki ya NMB yawanoa Mawakala wake Kanda ya Ziwa
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Meneja Kanda
ya Ziwa wa Benki ya NMB, Abraham Augustino (kushoto) akikabidhi cheti cha uwakala bora wa
Kanda hiyo kwa Suleiman Rwaikondo (kulia), katika kongamano la mawakala lililofanyika Jijini
Mwanza.
Baadhi
ya washiriki wa kongamano hilo.
Judith Ferdinand, BMG
Zaidi ya
mawakala 200 wa NMB kutoka Kanda ya Ziwa wamepatiwa mafunzo ya kujengewa uwezo
katika nyanja za huduma za kibenki, kudhibiti utakatishaji fedha haramu na
ulaghai, utoaji wa huduma bora kwa wateja pamoja na kukuza biashara na
ujasiriamali.
Mafunzo hayo
ambayo waliyapata katika kongamano la mawakala wa benki ya NMB lililofanyika
jana mkoani hapa lenye lengo la kuwaongezea ujuzi hili waweze kufanya kazi kwa
ufanisi.
Akitoa
mafunzo hayo Meneja Mahusiano, Kitengo cha Uwakala Makao Makuu Nehemiah Simba
alisema, utakatishaji wa fedha ni mfumo ambao wahalifu wanatumia kuweka pesa
ambazo ni haramu benki au kupitia mawakala, hivyo aliwataka washiriki kuacha
kufanya kazi kwa mazoea na watoe taarifa
pindi watakapokuwa na miamala ambayo
wanaitilia mashaka.
Kwa upande
wake Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya
Ziwa Abraham Augustino alisema, mafunzo hayo yatakuwa yanafanyika kila mwaka
ili kuwafanya mawakala kufanya kazi kwa ufanisi kwani lengo la kuwepo wao ni
kusogeza huduma za kibenki karibu na jamii.
"Kuwawezesha
mawakala kuwafungulia wateja wapya akaunti tofauti na ilivyo sasa, pamoja na
kufanya kazi ya kuweka na kutoa fedha huku watumishi wa benki wao
wakishughulika na utoaji mikopo," alisema Augustino.
Alisema, kwa
sasa wanamawakala 6000 nchi nzima ila malengo yao ifikapo mwaka 2020 wawe
20000,huku akiahidi kuwa benki hiyo itaabza kutoa mikopo kwao hili waweze
kujiendekeza katika biashara yao pamoja na kuangalia namna ya kuwapatia bima.
Akizungumza
kwa niaba ya washiriki wa kongamano hilo, Kalunde Kafiti aliushukuru uongozi
wa NMB kwa kuona umuhimu wao na kuamua kuwapatia mafunzo hayo ambapo
wamewaongezea elimu ambayo ni mtaji katika shughuli na biashara zao.
No comments: