LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wachimbaji wadogo Mkalama kupewa leseni zilizohodhiwa na wageni- Biteko

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Waziri wa Wizara ya Madini, Doto Biteko akiwasilisha salamu za Wizara hiyo kwenye mkutano wa hadhara wa Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan uliofanyika hii leo katika viwanja vya Halmashauri ya Mkalama mkoani Singida ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake mkoani humo iliyoanza Februari 16, 2019.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Waziri wa Wizara ya Madini, Doto Biteko akiwasilisha salamu za Wizara hiyo kwenye mkutano wa hadhara wa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan (wa kwanza kushoto) katika Halmashauri ya Mkalama mkoani Singida.
Waziri wa Madini, Doto Biteko amesema wizara hiyo inatarajia kuzifuta leseni 38 za utafiti wa madini zinazoshikiliwa bila kuendelezwa na wawekezaji wa kigeni katika Wilaya ya Mkalama mkoani Singida na kisha kuzigawa upya kwa wachimbaji wadogo.

Waziri Biteko ameyasema hayo leo wakati akitoa salamu zake kwenye mkutano wa hadhara wa Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, alioufanya katika eneo la Nduguti ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kikazi mkoani Singida aliyoianza Februari 16, 2019.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.