Watoto na vijana wako hatarini na vitendo vya ukatili "ubakwaji umetajwa"
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Imeelezwa
kwamba watoto na vijana wako katika hatari kubwa ya kukumbwa na vitendo vya
ukatili ikiwemo ubakaji, mimba na ndoa za utotoni hivyo wazazi na walenzi
wanapaswa kuangalia upya njia sahihi za malezi kwa makundi hayo muhimu katika
makuzi.
Mkurugenzi
wa shirika la kutetea haki za watoto na wanawake (KIVULINI) la jijini Mwanza,
Yassin Ally ameyasema hayo kufuatia kikao kazi cha wadau wa ukatili
kilicholenga kuandaa mikakati ya kuboresha upatikanaji wa huduma rafiki za afya
kwa vijana na wahanga wa ukatili.
Hatua hiyo
inalenga kusaidia utekelezaji wa mradi wa “sauti yangu, haki yangu katika
kupunguza mimba za umri mdogo Manispaa ya Ilemela” unaosimamiwa na shirika
hilo. Aidha mradi huo pia kusaidia utekelezaji wa mpango mkakati wa kiaifa wa
kutokomeza ukatili dhidi ya watoto na wanawake (MTAKUWWA) kwa asilimia 50 hadi
ifikapo mwaka 2021/22.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: