LIVE STREAM ADS

Header Ads

Naibu Waziri wa Nishati atoa miezi sita kwa wakandarasi

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amemtaka mkandarasi kampuni ya NIPO Group kuhakikisha ifikapo Juni 30, 2019 awe amesambaza umeme katika Vijiji vyote vilivyopo Wilaya Sengerema mkoani Mwanza.

Mgalu alitoa agizo hilo Disemba 21, 2019 wakati akiwasha umeme katika Kijiji cha Kanyala Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema na kuongeza kwamba agizo hilo linapaswa kutekelezwa pia na wakandarasi wengine kote nchini.

Aidha Mgalu alibainisha kwamba Serikali imetenga shilingi bilioni 179 ili kutekeleza mradi wa Ujazilizi kuanzia mwezi Januari 2020 katika mikoa tisa nchini ikiwemo Mwanza kwa ajili ya kufikisha nishati ya umeme katika maeneo ambayo hayakupata nishati hiyo kupitia mradi wa REA.
Tazama BMG TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.