LIVE STREAM ADS

Header Ads

Sengerema ‘wavuvi kambi ya Mchangani walilia umeme’

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Wavuvi katika kambi ya Mchangani iliyopo Halmashauri ya Buchosa Wilaya Sengerema mkoani Mwanza, wameiomba Serikali kuwafikishiwa nishati ya umeme ili waweze kuboresha zaidi shughuli zao za mazao ya uvuvi.

Wavuvi hao walitoa ombi hilo Disemba 21, 2019 mbele ya Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu aliyefanya ziara ya kukagua miundombinu ya umeme na kuzindua nishati hiyo katika Halmashauri ya Buchosa kupitia mradi wa umeme vijijini REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza.

Akijibu ombi la wavuvi hao, Mgalu alisema Wizara yake itawasiliana na Wizara ya Maliasili na Utalii ili kupata mwafaka ikiwa kambi hiyo ya Mchangani inayozungukwa na pori la msitu wa Kisiwa cha Kome inaweza kufikishiwa nishati ya umeme.
Tazama BMG TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.