LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wanawake Misungwi waitumia vyema mikopo kujikwamua kiuchumi

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.co
 Wanawake katika Wilaya Misungwi mkoani Mwanza wametajwa kuitumia vyema mikopo inayotolewa na Halmashauri kujikwamua kiuchumi huku pia wakiwa warejeshaji wazuri wa mikopo hiyo ikilinganishwa na makundi mengine.

Hayo yalibainishwa na Mratibu wa dawati la uwezeshaji wanawake kiuchumi wilayani humo kwenye kongamano la wanawake ikiwa ni sehemu ya shughuli kuelekea kilele cha siku ya wanawake duniani ambayo kitaifa mwaka huu 2020 yatafanyika mkoani Simiyu.

Tangu mwaka 2018 hadi Machi 2020 Halmashauri ya Wilaya Misungwi imetoa shilingi Milioni 298 kama mikopo isiyo na riba kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa ajili ya kuanzisha miradi mbalimbali lakini baadhi ya vikundi vinaelezwa kutumia ndivyo sivyo fedha hizo na hivyo kushindwa kurejesha mkopo.

Kongamano hilo liliandaliwa na shirika la kutetea haki za wanawake na wasichana KIVULINI huku kauli mbinu ya maadhimisho ya Siku ya Wanamke Duniani ambayo huadhimishwa Machi 08 kila mwaka ikiwa ni “Kizazi cha Usawa kwa Maendeleo ya Sasa nay a Baadaye”.
#BMGHabari
 Mkurugenzi Mtendaji wa KIVULINI, Yassin Ally akizungumza kwenye kongamano hilo.
 Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa Mwanza, Isack Ndasa akizungumza kwenye kongamano hilo ambapo alitoa rai kwa vikundi vinavonufaika na mikopo ya Halmashauri kuitumia vyema mikopo hiyo na kuirejesha kwa wakati badala ya kuitumia kwa anasa.
Baadhi ya wanawake wilayani Misungwi waliohudhuria kongamano hilo.
Tazama BMG TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.