Ndege ya mizigo kuimarisha usafirishaji samaki nje ya nchi
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema mipango ya
Serikali kununua ndege ya mizigo utaimarisha usafirishaji wa minofu ya samaki moja
kwa moja kwenda nje ya nchi kutokea uwanja wa ndege wa Mwanza.
Waziri
Kamwelwe ameyasema hayo Jumatatu Juni Mosi 2020 jijini Mwanza wakati akifungua
mkutano wa kupokea mikakati ya pamoja kuondoa vikwazo na kufanikisha biashara ya
usafirishaji minofu ya samaki kwenda nje ya nchi hususani mataifa ya Ulaya
ambako kumekuwa na soko la uhakika.
Mkutano huo umewajumuisha pia Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Wizara za Mifugo na Uvuvi,
Viwanda na Biashara pamoja na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa ya
Kanda ya Ziwa.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe (katika) akizungumza kwenye kikao hicho. Kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa na kulia ni Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella.
Tazama BMG ONLINE TV hapa chini
SOMA>>> Habari zinazohusiana
No comments: