LIVE STREAM ADS

Header Ads

Biteko achachamaa ‘mgodi wa Mwadui kuuzwa kinyemela’

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

 Waziri wa Madini, Doto Biteko ameutaka uongozi wa mgodi wa almasi wa Mwadui (Williamson Diamond Ltd) hadi kufikia Ijumaa Julai 10, 2020 uwe umewasilisha taratibu zilizofuatwa kabla ya kutangaza kuuza mgodi huo bila kuishirikisha Serikali ambayo ina ubia wa asilimia 25.

Biteko ametoa agizo hilo Jumapili Julai 05, 2020 wakati akizungumza na Menejimenti ya mgodi huo uliopo Maganzo Wilaya Kishap mkoani Shinyanga huku akieleza kusikitishwa na taarifa ya mgodi huo kuuzwa aliyoipata kupitia tangazo lililotolewa mtandaoni bila kuishirikisha Serikali.

Mbali na kuomba taarifa kuhusiana na mgodi huo kuuzwa, Biteko pia ametaka kupewa taratibu za kikazi zilizofuatwa kabla ya kuwasimamisha baadhi ya wafanyakazi wake kwa kigezo cha kusitisha uzalishaji ili kufanya matengenezo ya moja ya mitambo wa kuchenjua almasi.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Tazama BMG ONLINE TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.